Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo BREAKING news. Onyesha machapisho yote
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo BREAKING news. Onyesha machapisho yote

Jumapili, 5 Machi 2017

PICHA: Ajali ya Mabasi iliyotokea Mlima Kitonga



IRINGA: Basi la Abood lililokuwa likitokea Iringa kwenda Dar es Salaam limeligonga kwa nyuma basi la Happy Nation lililokuwa likitokea Mbeya kwenda Dar es Salaam kwenye milima ya Kitonga ambapo basi hilo liligonga lori la mizigo aina ya Fuso.

Katika tukio hilo mabasi hayo mawili yalitumbukia kwenye korongo lakini taarifa ya kifo au majeruhi bado hazijapatikana.

Ijumaa, 3 Machi 2017

Ujumbe kutoka kwa Mbunge wa Arusha mjini . Godless Jonathan Lema leo



Mheshimiwa Lema ameshukuru Mungu kwa maana ametenda juu yake, amemshukuru mkewe na kusema angepata bahati ya kuoa angemuoa tena mke wake tena kwa ujasiri alioonyesha kwa kipindi chote na kuishukuru familia yake.

Pia ameshukuru viongozi wote wachama na wanachama pamoja na wananchi wake wa Jimboni Arusha na watanzania kwa ujumla. Amesema hana mengi ya kusema bali atazungumza kupitia Waraka wake kwa Rais atakao toa hivi karibuni, pia ameomba kupumzika na familia yake hasa kwenda kumuona mtoto wake ambae aliwahi muuliza "Baba ni kosa gani na Mimi naweza Fanya ili nikae na wewe huku gerezani?"

Amesema ameongeza hari ya mapambano dhidi ya Dola.
My take ==Kuna watu wanauma sana meno, na wamenuna hasa baada ya Lema leo kutoka! Kwa Mungu ni zaidi ya ushindi hata kama binadamu hawapendi.
=============
Mapokezi nyumbani kwake muda huu
tmp_31279-IMG-20170303-WA0018-365232814.jpg 
tmp_31279-IMG-20170303-WA00271320963016.jpg 
tmp_31279-IMG-20170303-WA0025994258838.jpgtmp_31279-IMG-20170303-WA00261454842015.jpgtmp_31279-IMG-20170303-WA0024407360187.jpg

Kutoka Mahakamani: Mbunge wa Arusha Godbless Lema apata dhamana

Mahakama Kuu Kanda ya Arusha leo inatarajiwa kutoa uamuzi kuhusu maombi ya dhamana ya Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema.

Ni asubuhi tena kwa mbali jua limeanza kuchomoka huku Arusha ikiwa ni siku ya kupatiwa haki kwa Mbunge wa Arusha mjini Godbless Lema baada ya kuwekwa kizuizini kwa takribani miezi ninachoamini ni kwamba Mahakama kuu leo itatenda haki kwa Lema

Ulinzi nje eneo la mahakamani umeimarishwa sana.
Wananchi wamezuia kuingia mahakama kwenda kusilikiza kesi ya Mbunge wa Jimbo la Arusha Mjini Godbless Jonathan Lema.

Waandishi wa habari wawili tukiwa nje ya eneo la mahakamani tumekamatwa na Jeshi la Polisi .tumeshikiliwa kwa muda lisaa baada ya majadiliano wahusika tumeachiwa tumezuia kuingia mahakamani.

Mbunge wa Jimbo la Arusha Mjini Godbless Jonathan Lema akishuka kwenye gari kuingia mahakamani.

Nje eneo la mahakamani wananchi zaidi 23 wamekamatwa na Jeshi la Polisi muda huu wakiwa nje la mahakamani baada ya kuzuiwa kuingia mahakamani kusilikiza kesi ya Mbunge Godbless Jonathan Lema.

Kutoka mahakamani
Wakili wa Serikali ameomba dakika 15 kuwasilisha hoja na Wakili Msomi Peter Kibatala amekubali na kuomba wapewe saa 1 kujibu so Mahakama imehairishwa mpaka saa 7 mchana

Kutoka mahakamani "Virungu vinatembea mahakamani muda huu,watu wanapigwa ,wengine wamekamatwa wamepelekwa central.
Magari ya kuwasha,police wapo na silaha nzito.

Watu wamezuiliwa kuingia,maeneo ya nje ya mahakama ni virungu".

tmp_23435-FB_IMG_14885247387692090696793.jpg 
Viongozi mbalimbali wa Chadema wakiongozwa Katibu Mkuu wa Chadema Dr Vicent Mashinji, Waziri Mkuu Mstaafu na Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema Edward Lowasa, Waziri Mkuu Msaatafu Sumaye na Meya wa Jiji la Arusha Mjini Kalisti Lazaro wakiwa mahakamani .
tmp_23435-FB_IMG_1488525644504-1345217214.jpg
Mwenyekiti wa Chadema Taifa Freeman Mbowe Naibu Katibu Mkuu Chadema John Mnyika ,pamoja na Viongozi mbalimbali wakiwa mahakamani leo.
View attachment 476314 
tmp_7995-FB_IMG_14885273469431093721955.jpg

Viongozi Wakuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), wakiwa nje ya Mahakama Kuu ya Arusha baada ya Mawakili wa Jamuhuri kuomba kuwasilisha hoja ambayo wamekwenda kuiandaa kwa dakika 15 na Jopo la Mawakili wa Utetezi likiwakilishwa na Wakili Msomi Peter Kibatala,wameomba dakika 60 ili kujiandaa kujibu hoja hiyo ya mawakili wa Jamuhuri..
tmp_13412-FB_IMG_1488537019231711232815.jpg
Mahakama Kuu Arusha inatarajia kutoa maamuzi ya dhamana na Godbless Lema saa saba na nusu mchana. Mawakili wamepewa muda kujibu hoja zilizotolewa.

Viongozi mbalimbali wa Chadema wanaanza kuingia mahakamani kusubiri uamuzi wa Jaji Magimbi kuhusu dhamana ya Mbunge Godbless Jonathan Lema.

Mahakama Kuu Kanda ya Arusha Mjini baada ya kupitia hoja za mawakili pande zote imemwachia kwa dhamana Mbunge wa Jimbo la Arusha Mjini Godbless Jonathan Lema. Ameachiwa kwa dhamana ya masharti ya wadhamini wawili na kusaini bondi ya shilingi milioni moja.

Jumatano, 1 Machi 2017

Vita ya Dawa za Kulevya: Steve Nyerere alivyopiga kambi Bungeni Kumuokoa Wema Sepetu

1. Steve Nyerere ndiye aliyewapa Mwigullu, Nape, Msukuma na Mlinga namba za simu za Mama Wema Sepetu

2. Nape na kundi lake waliapa kupambana na Makonda bila kumshirikisha Wema kwa vile ni mropojaji , angeweza kutoa siri. Lakini siyo siri tena.

3. Nape walifikiri kufanya hivyo ni kumuokoa Wema kwa vile alikitetea Chama wakati wa uchaguzi. Wakasahau kuwa wanakidhalilisha Chama kutetea wauza Unga tofauti na ilani ya Chama inavyosema

4. Kwa upande wake Steve Nyerere alijua akimuokoa Wema, CCM wangerudi kumbembeleza Wema kupitia kwake na hivyo angepiga pesa za kutosha

5. Steve Nyerere aliwafikia pia Wabunge wa CHADEMA wakiwemo Freeman Mbowe na Zitto Kabwe ndiyo maana Bunge lilipuka
Mytake: 1. Nape , Mwigullu wanapaswa kujitathmini kama wanastahili kuendelea kuwa viongozi waandamizi wa serikali ? Nini hatma ya Nape, Mwiggulu na Msukuma ndani ya CCM?

2. Mwigullu, Nape na Msukuma ni wana CCM waliokuwa maadui namba moja wa CHADEMA, Je Chadema wamefanikiwa kuwamaliza kisiasa? Je wanaweza kuwapokea ndani ya CHADEMA endapo CCM wataamua kutokuwa na imani nao kwa kitendo chao cha kuunganna na Wabunge wengine wa CHADEMA kutetea watuhumiwa wa madawa ya kulevya na hivyo kudhoofisha juhudi za serikali ambayo wao ni sehemu ya serikali katika kupambana na bishara ya dawa za kulevya?

3. Kwa ujumbe wa huu wa sauti kati ya Mama Wema Sepetu na Steve Nyerere na kwa kuzingatia nafaai za Nape na Mwigullu, hawapaswi kujiuzulu ili kulinda heshima ya serikali?

Attached Files:

nafasi za kazi TTCL,ingia kuziona


Details
Employer Name: Tanzania Telecommunication Company Limited
Role: Management
Position Type: Full Time
Location: Dar Es Salaam
                    Other Dar es Salaam District
Application Deadline: 06-03-2017
Description
Job Ref No: 3121000
Job Title: Revenue Officer
Post(s): 1
Report To: Treasury Manager

Objectives:
Effective and efficient management of the Company’s revenue records and maintenance of a robust revenue and receivables accounting system for all services offered by TTCL.

Key Responsibilities:

1. Timely production of an accurate Trial Balance and transactions reports.
2. To ensure preparation of monthly reconciliation of all key accounts
3. To ensure proper and timely bookings of all manually processed payments voucher are done within the cut off period after payment.
4. To ensure supplies remittance advise are obtained following the payment made
5. To ensure monthly payments made reconcile with cheque list, suppliers’ accounts and bank accounts following the payments.
6. To ensure that all payments run are done in proper periods; with proper reference numbers within the month of payment.
7. To Ensure proper financial records are kept and accounting procedures and policies are implemented and followed across all centres in the regions and head office
8. To ensure balance sheet reconciliation are formed on a monthly basis.
9. Perform any other business tasks as directed by the Treasury Manager or other senior officials of the Company.

Key Qualifications / Experience / Skills:

• Degree/Advanced Diploma in Accounting/Finance/Commerce or Business Administration majoring in Accounting/Finance/Commerce.
• CPA (T), ACCA or equivalent qualification recognized by the National Board of Accountants and Auditors (NBAA).
• At least two (2) years experience in finance activities.
• Excellent interpersonal and communication skills, along with ability to develop and sustain effective teamwork.
• Computer knowledge in Microsoft Applications and Sun Systems Accounting Software package.
• Excellent communication and interpersonal skills.
• Able to work in teams.
• Analytical and attention to detail.
• Able to meet reporting deadlines.

Daladala ya Mbagala yapata ajali Kigambon

Basi iloangukia daraja la mwongozo Kigamboni leo hii
013330e1-ad9f-462c-8810-d9981dc6278e.jpgfef9b80e-8bef-4aef-a56c-f2d0b4cb8564.jpgcd5ed7c2-5d10-48a4-91dd-fca4e9f7340c.jpg 
Ntawaletea habari zaidi

Rais Magufuli amteua Bi. Salma Kikwete kuwa Mbunge

TAARIFA KIVA VYOMBO VYA HABARI

Ikulu, Dar es Salaam.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli, leo tarehe 01 Machi, 2017 amemteua Mhe. Salma Kikwete kuwa Mbunge wa Viti Maalum wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Mhe. Salma Kikwete ni Mke wa Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete.

Mhe. Salma Kikwete ataapishwa kwa mujibu wa sheria na taratibu zitakazotangazwa na Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais,IKULU
01 Machi, 2017

Dar es Salaam
[​IMG]

Masahihisho ya Ikulu:

Mama Salma Kikwete ameteuliwa kuwa Mbunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na SIO Mbunge wa Viti Maalum

Job seekers jihadharini na hawa matapeli


connymarty
Wamewaita watu kwenye interview halafu wanataka kuwatoza ela ya kufanyia iyo interview ambayo ni 16,500 tena wanakuambia uwatumie through airtel money ambapo wanakutumia email na pia sms ikikuambia ufungue email yako na interview iyo wanasema itafanyika tarehe 4/3/2017 so sambazeni ujumbe huu
na email yao inasema ivi

Hi Applicant!

I have the pleasure to inform you that the RECRUITMENT DEPARTMENT TEAM has received, reviewed and thoroughly discussed your credentials and has finally made a decision of calling you for a face to face interview.

BRIEF INTRODUCTION TO R.I.F.A CONSULTANTS CO. LTD

(Recruitment Department)
We are a general Consultancy firm with superb experience and expertise in almost all areas of consultancy with a base in Dar es salaam Tanzania - (OUR OFFICE IS LOCATED AT OHIO STREET - CLOSELY ADJACENT TO BARCLAYS BANK HOUSE - POSTA DAR ES SALAAM)

We conduct numerous operations in Tanzania and East Africa as a whole and indeed enjoy a very huge and healthy client database.

Due esteemed and outstanding services,have given us a chance to command and enjoy an extra-ordinary bigger market share in the consultancy field since our inception in February, 2010! We simply embrace and cherish excellent services with diligence.

ABOUT THESE POSTS AND THE EMPLOYMENT ARRANGEMENT:

We are recruiting ON BEHALF OF THE CLIENT (Heron Food Supermarket) this means that you will meet OUR CLIENT (who in this case will be your employer) on the Interview table come Saturday Fourth of March, 2017!

All candidates will be informed on the spot and all the allocation discussions and arrangements will be taken care of by the Employer.

INTERVIEW DATE / VENUES:

1. 04/03/2017 - KARENA HOTEL - SHINYANGA TOWN - (ask for the interview Hall by the entrance gate or call this number +255 686 479 958 on interview date for more clarifications.

2. 04/03/2017 - CCM MKOANI HALL - DAR ES SALAAM REGION - (ask for the interview hall by the entrance gate or call this number +255 686 479 958 on interview date for more clarifications.

3. 04/03/2017 - CCM MKOANI HALL - DODOMA REGION - (ask for the interview hall by the entrance gate or call this number +255 686 479 958 on interview date for more clarifications.

4. 04/03/2017 - CCM MKOANI HALL -MOROGORO REGION - (ask for the interview hall by the entrance gate or call this number +255 686 479 958 on interview date for more clarifications.

5. 04/03/2017 - MEATU HOTEL - SINGIDA REGION - (ask for the interview hall by the main entrance or call this number +255 686 479 958 on interview date for more clarifications.

6. 04/03/2017 - CCM MKOANI HALL - TANGA REGION - (ask for the interview hall by the main entrance or call this number +255 686 479 958 on interview date for more clarifications.

7. 04/03/2017 - CCM MKOANI HALL - ARUSHA REGION - (ask for the interview hall by the main entrance or call this number +255 686 479 958 on interview date for more clarifications.

8. 04/03/2017 - CCM MKOANI HALL - MBEYA REGION - (ask for the interview hall by the main entrance or call this number +255 686 479 958 on interview date for more clarifications.

9. 04/03/2017 - NGASAMO HOTEL - RWAGASORE STREET - MWANZA CITY - (ask for the interview hall by the main entrance or call this number +255 686 479 958 on interview date for more clarifications. 

10. 04/03/2017 - CCM MKOANI HALL- PWANI REGION - (ask for the interview hall by the main entrance or call this number +255 686 479 958 on interview date for more clarifications. 

11. 04/03/2017 - CCM MKOANI HALL- MTWARA REGION - (ask for the interview hall by the main entrance or call this number +255 686 479 958 on interview date for more clarifications. 

TIME: 

All interviews will be conducted from 09:00 A.M to 04:00 P.M in all the stated venues concurrently 

NOTE:
1. WE WILL RUN 11 INTERVIEWS IN THE ELEVEN VENUES AT THE SAME TIME, SAME DATE!

2. MAKE SURE YOU GO TO ANY OF THE STATED VENUES AT THE RIGHT TIME
INTERVIEW SESSIONS:

1. Written interview - 1st. Session

2. Oral Interview - 2nd. Session

3. Verification of all the Certificates 3rd. Session

REQUIREMENTS:

1. All Original Certificates / Testimonials

2. Those with copies of the Original Certificates MUST LEGALLY VERIFY THEM. (Only genuine cases will be considered)

3. Those with Transcripts MUST COME WITH STAMPED ONES FROM THE RESPECTIVE 

INSTITUTIONS

4. Voter's Id plus Birth Certificate (not a must but very important)

REGISTRATION CRITERIA:

1. ALL APPLICANTS ARE REQUIRED TO REGISTER WITH TSHS. 16,500, ONLY - this amount should be sent to AIRTEL MONEY ACCOUNT NO: +255 783749091 (RIFA CONSULTANT LTD / RECRUITMENT DEPARTMENT) BEFORE OR ON THURSDAY 02/03/2017 by 7:00 P.M- (SAA MOJA JIONI)

NOTE:
This amount of money will cover the following;

1. Consultation fees for the whole Employment and Job-Search process

2. Interview allowances for all our INTERVIEWERS/ SPECIALISTS who will be spread across all REGIONS

3. We DO NOT ASK FOR ANY DEDUCTIONS FROM YOUR SALARY ONCE YOU GET EMPLOYED UNLIKE OTHER JOB-SEARCH COMPANIES and that is why we are well connected with International NGOs, COMPANIES, INSTITUTIONS all over EAST, CENTRAL, SOUTHERN AND WESTERN AFRICA!!

4. Stationery (pens, foolscap, clipboards plus venue charges ).
NOTE: PLEASE COME FOR THE INTERVIEW WITH THE AIRTEL MONEY TRANSACTION TEXT FOR VERIFICATION!

--
Mr. ABUBAKHAR GONDWE
RECRUITMENT DEPARTMENT AND LOGISTICS IN CHARGE
R.I.F.A CONSULTANTS CO. LTD
DAR ES SALAAM-TANZANIA.

Kamanda Mpinga mchukulie hatua kali msanii Ali Kiba kwa kuvunja sheria za barabarani

Kwako Kamanda Mpinga,



Msanii Ali Kiba amefika nchini leo akitokea Afrika Kusini. Baada ya kufika uwanja wa kimataifa wa Mwalimu Nyerere alipokelewa na mashabiki wake.

Katika hali ya kushangaza msanii huyo amepanda juu ya gari na kushikilia tuzo yake kujigamba kwa mashabiki wake.

Kitendo hiki kinahatarisha maisha yake na maisha ya wengine wanaotumia barabara. Hatari hiyo ni zaidi ya kutofunga mkanda, kuendesha gari lisilo na breki, tairi lenye kipara etc.

Sheria za usalama barabarani haziruhusu ujinga huu hivyo msanii huyu achukuliwe hatua kali sana.

Kitendo alichokifanya ni zaidi ya dereva wa Itigi au Diamond Platnumz.

Jela inamnukia.

Konyagi wakaidi agizo la Serikali, waendelea kuzalisha 'Viroba'

Waziri Makamba na timu ya TRA, Polisi,TFDA na NEMC wavamia kiwanda cha konyagi na kukuta viroba vilivyopigwa marufuku vikitengenezwa.

Screenshot from 2017-03-01 15-01-44.png

wafahamu wa ghana alio isumbua idara ya usalama wa marekani kwa miaka 10


Sept mwaka jana ilikuwa mara yangu ya kwanza kukanyaga ardhi ya Marekani. Kuna vitu viwili-vitatu nikuwa navifanya pale Arlington City, Washington DC.
[​IMG]
Nikiwq nakatiza mitaa ya Crystal City, DC.

Nikiwa na mwezi mmoja tu tangu nimalize shahada yangu ya UDSM, sikuwa na familia (mke + watoto), sikuwa na assets kama hati ya nyumba, shamba, kiwanja na kadhalika, hivyo nilipitia vikwazo vingi sana hadi kupatiwa visa ya Marekani. Kitu kimoja kilichonisaidia ni kwamba nilikuwa nimesajili kampuni ya biashara, operations zilikua zimeanza miaka miwili iliyopita, na account ya biashara ilikuwa ina digits zisizo na shaka, biashara ilikuwa tayari ina assets za kutosha za kuprove kuwa lazima nitarudi nchini. Hivyo nikafanikiwa kuwa granted visa ya Marekani daraja B-1/B-2.[​IMG]

Kimsingi ili kupata visa ya US inabidi uthibitishe beyond reasonable doubts kuwa ukisafiri kwenda US utarudi nchini kwako ndani ya muda uliopanga na si kuzamia.

Process nzima ya kupata visa haikuwa lelemama, ulikuwa ni mchakamchaka ambao kiukweli unanyima usingizi.

Tuendelee...

Kwanza kabisa niseme tu wazi, mimi ni 1st generation katika familia/ukoo wetu kwenda US, hivyo sikuwa na guidance yoyote, sikufahamiana na mtu yoyote ambae angeweza kuniongoza, sikuweza kufetch experience yoyote, hivyo ilinilazimu nikomae kivyangu.

Process ya kupata Visa ilianza kwa kujaza online form inayoitwa DS 160 iliyopo kwenye web ya embassy ya Marekani. Ile form ni ndefu sana, ina maswali mengi mno, mengi yalikuwa ni very technical na ya kiintelijensia sana. Niliumiza kichwa sana kuhakikisha naijaza kwa umakini. Nilitumia karibu siku 5 hadi kuisubmit - hata kabla sijaisubmit niliirudia mara 10_10.

Baada ya kusubmit hatua iliyofuata ilikuwa kwenda Citi bank ipo pale Posta, nikalipa $160. Baada ya kulipa nikapata codes fulani ambazo nilizitumia kuomba interview slot. Nakumbuka siku ya interview niliomba iwe Jumatano saa 2 asubuhi.

Hapo tayari nimeshapata tetesi jinsi ambavyo Waafrika wananyimwa visa ya Marekani, nikaGoogle kwamba Marekani wanaingiza $56 mil kila mwaka kutoka Afrika kwa visa vinazokataliwa. Nilikuwa na hofu kubwa sana, hasa nikizingatia nilikua kipindi ambacho sitaki kupoteza hata 'Jero'.

Siku ya interview nikajiandaa vizuri sana, tayari nimekunywa nondo za kutosha kutoka Google, nikabeba makabrasha na documents zangu zote, nikavaa kiheshima haswaa (vijana wa kileo wanasema 'mapigo ya kifaza'), nikafika pale embassy hata kabla ya muda (kuzuga kuonesha kuwa sina mambo ya kiafrika ya kuchelewa).

Pale nilipigwa search ya kufa mtu, nikaacha vitu vyote security nikaingia sehemu ya kusubiri interview. Ni eneo la wazi ambapo watu wote waliopangiwa kufanya interview siku hiyo wanakaa.

Tuliokuwa na interview siku hiyo tulikuwa kama watu 30, kulikuwa na msanii mmoja maarufu (sitamtaja jina), pia alikuwepo mtoto mmoja maarufu wa Raisi Nyerere na pia alikuwepo jamaa mmoja wa TISS ambae yeye alitumwa na waziri fulani (huyu jamaa hakupitia process zozote, aliweka documents zake pale pa'kufanyiwa interview, akapewa maelekezo kisha akasepa).

Kabla interview hazijaanza tuliweka kaplatform uchwara tukawa tunadiscuss mambo kadha wa kadha hasa uchaguzi wa US. Yani mimi ndio nilijiona kilaza, kuna jamaa anajua vitu vyote inside-out vinavyoihusu US na blah blah kibao. Alikuwa anamwaga nondo kuhusu Marekani, miji yake, utamaduni wa Wamarekani, Siasa za marekani, akaanza kutoa 'tips' za maswali ya interview ya kupata visa (nilikuja kugundua kuwa huyu jamaa ni member humu JF - japo sikuweza kung'amua identity yake). Hakika Huyu jamaa alinipa hofu sana, nilihisi kwa nilivyo 'shallow' lazima nitanyimwa Visa - nikajipange vizuri zaidi.

Pia kuna mama mwingine tulikuwa nae akawa anasema alivyojaribu kuomba visa na kunyimwa kila mara, ile ilikuwa mara yake ya 5 anaitwa kwenye interview. (Kumbuka: ukiwa rejected kwenye interview, inabidi urudi uanze application upya na utalazimila kulipa $160 upya), kwa mantiki hiyo, mama yule tayari alitumia $640 kuapply visa). Swala la huyu mama liliniongezea hofu, sikutaka tena story za kijiwe cha mule ndani. Nikajitenga pembeni nikachukua vitabu fulani vya utalii vilikuwa pale nikawa nasoma soma.

Sasa muda wa interview ukaanza, mtu mmoja mmoja anapita kwa ndani kidogo, kuna kidirisha (kama bank kwa teller), then anaanza kuhojiwa na wafanyakazi wa pale embassy. Mtu anayekubaliwa visa basi analazimika kuacha passport yake pale na kupangiwa tarehe ya kuja kuchukua visa yake. Asiyekubaliwa anapewa vitu vyake vyote aondoke navyo.

Katika watu 30, mimi nilikuwa wa 23. Watu wengi walionitangulia walikuwa wananyimwa visa, wengine hadi wanalia pale dirishani. Kiukweli kwenda US ni kama 'dream come true' kwa sisi ambao tulitokea 'the other side of poor neighbourhoods'.

Yule jamaa wa JF aliyekuwa anajua vitu vyote vya States akafika pale dirishani akiwa na mbwembwe nyingi, anapiga kingereza kidogo kisicho na kigugumizi tofauti na mimi. Sikuweza kusikia mahojiano yao, lakini Kitu kilichonistua yule jamaa alirudi na passport yake mkononi, kuashiria kua amenyimwa visa. Pale matumaini ya kupata visa yakaniishia kabisa, moyo ukafadhaika sana. Yule mtoto wa Nyerere aliacha passport yake pale, lakini pia yule msanii alinyimwa.

Zamu yangu ikafika. Moyo ulikuwa unatokota na uwoga 'si wa nchi hii'. Nilivyofika pale dirisha la interview yule jamaa akagundua nina hofu ya hali ya juu sana.

Mahojiano yakaanza. (Hapo ninatetemeka kwa hofu na woga).

Consular: Morning!

Mimi: Yes! Morning

Consular: Akatabasamu kidogo, kisha akauliza - Your sir please!

Mimi: Nikiwa sijitambui nikajibu - Yes sir please .

Jamaa akasmile tena, akaniuliza kwa kiswahili cha kuunga unga. Aiseee!! Hapo nilifunguka si mchezo.

Tulivyoendelea na conversation ndivyo nilivyozidi 'kugain momentum' hadi nikawa kwenye hali yangu ya kawaida.

Statement ya mwisho ikawa "Congratulation sir, you've been granted the US visa, leave your passport with me, and you'll collect it tomorrow together with your visa". Aisee! Feeling ile ilikuwa ya kipekee sana sana. keshowe nilivyokuja kuchukua visa tulikuwa watu wanne tu kati ya wale 30 tuliofanyiwa interview.

Lakini still baada ya kupata visa yangu nilijiuliza sana kwanini US inatubania kupata visa zao?
Kwanini processes ni nyingi mno? kwanini gharama ni kubwa mno?
Je hakuna alternative ya kuingia US bila usumbufu wote huo?

After all sikujali sana kwa sababu tayari nilishapata visa yangu, na vile isingenisaidia kitu kuhoji masharti kila nchi inayojiwekea katika kukaribisha wageni.

Lakini kitu kilichonishangaza zaidi ni wakati nilipofika DIA - Dulles International Airport.

Nikiwa kwenye foleni wakati wa passport control nikamuona black mmoja kasimamishwa muda mrefu sana pale dirishani kwa 'immigration official', lakini white walikua wanapita fasta sana (hata hawakuchukua zaidi ya dakika 1).[​IMG]

Zamu yangu ikafika. Nilipofika tu pale dirishani jamaa kwanza aliniangalia usoni kwa sekunde kadhaa na mimi nikamkazia jicho, 'mubashara' (live) kabisa bila kupepesa kope. Akaniomba passport, nikampa. Akaipitia page baada ya page - kisha akaniuliza "What took you to all these countries?". Kwasababu nilijua nipo 'clean' na nina makaratasi yote muhimu, nikamjibu kwa dharau "I cleared it out when I was in those countries, now I'm in the US - ask me about US". Jamaa akaScan kwanza passport yangu, then akaendelea kunihoji maswali yake ya kiintelijensia. Mimi wala sikutaka kuongea sana, hasa ukizingatia ngeli imekaa kushoto , nilichokifanya ni kumjibu kila swali kwa maelezo machache na kumpa makaratasi. Nilikaa pale kwa dakika 16 - to be exact.[​IMG]

Nilivyoruhusiwa nilijiuliza sana, kwanini hawa jamaa wako 'so arrogant' na nchi yao na wanadharau sana. Nilitamani na sisi waAfrika tuwe na kauwezo ka kuwashikisha adabu na kuwakomoa hawa jamaa.[​IMG] Muonekano wa nje kutoka kwenye dirisha la hotel room nilipofikia

Watoto wa Accra wakanipa sababu ya kuwadharau Marekani na vyombo vya ulinzi na usalama.

Jumanne Nov 8 2016 dunia yote ikielekeza macho kufuatilia uchaguzi mkuu wa Marekani. kuna jambo kubwa sana lilitokea Accra ambalo lilikosa 'Air time' mubashara kutokana na media zote kuelekeza nguvu kwenye uchaguzi mkuu wa uraisi. Tukio hili la kustaajabisha, lililosukwa kwa akili kubwa sana na wahuni wa Ghana, na lilinipa sababu ya kuwaona Wamarekani ni 'watupu'.

Kwa zaidi ya muongo mmoja bendera ya marekani ilikuwa inapeperushwa nje ya jengo kuu-kuu la rangi ya pink katikati ya mji mkuu wa Ghana, Accra.

Mgeni yeyote aliyeingia ndani ya jengo hilo alikutana na picha kubwa ya Rais Barack Obama ikining'inia ukutani. Mapokezi-mezani kulikuwa na kitabu cha wageni chenye seal halali ya idara ya ulinzi ya Marekani. Kila mgeni alikabidhiwa coupon yenye maelekezo, na mwisho kulikuwa na maandishi "Welcome to the US embassy in Ghana".[​IMG]

kijana machachari na mipango ya kibabe

Mwaka 2004 kijana wa umri wa miaka 23 aitwae Yaw Kwabedo anahitimu shahada ya sheria ya chuo kikuu cha Ghana - idara ya sheria. Alihitimu akiwa mmoja wa wanafunzi wenye ufaulu wa juu zaidi darasani kwake.

Kama ilivyo kwa vijana wengi wa Afrika Magharibi, Yaw alikua na ndoto na matamanio ya kwenda na kufanya kazi Marekani kama mshauri wa masuala ya kisheria katika makampuni makubwa.

Aliandaa makabrasha yake yote muhimu, kisha akaanza mchakato wa kupata visa ya Marekani. Aliomba visa mara 4 lakini alinyimwa, alipoteza kiasi kikubwa cha pesa lakini bado aliziishi ndoto zake. Ilimbidi auze baadhi ya mali za nyumbani kwao ikiwemo simu pamoja na runinga, kisha akaomba visa kwa mara ya 5. Lakini bado hakufikia vigezo, akanyimwa tena. Aliumia mno.

Kwabedo aliamini fika kuwa Ubalozi wa Marekani umemdharau na kumdhalilisha. Hivyo, 'piga - uwa - galagaza' atafanya kila awezalo kulipiza kisasi ambacho aliamini lazima angeidhalilisha marekani katika uso wa dunia. Aliapa gharama zake zote alizotumia kuomba visa na kunyimwa zingerudi, pamoja na fidia juu. Aliapa kuwawezesha waghana wote watimize ndoto zao za kuishi Marekani.

Kisasi kinasukwa kwa ustadi wa hali ya juu sana

Feb 2005, Yaw akiwa anatimiza miaka 24 alimwita rafiki yake wa karibu ambaye alihitimu mafunzo ya uhandisi wa kompyuta, kisha akamshirikisha wazo lake ambalo lililenga kuidhalilisha Ubalozi wa Marekani, Idara ya ulinzi na usalama pamoja na vyombo vya kiintelijensia vya Marekani. Huyu rafiki alisita sana akihofia uwezo na nguvu waliyonayo Maafisa wa ulinzi wa Marekani. Lakini Yaw alifanikiwa kumshawishi, na wakaendelea na mipango.

Yaw alihitaji funding, hivyo aliwaingilia watu wenye uhasama na Marekani na kuwashirikisha mpango wake, aliwaendea Waturuki, akawafafanulia vizuri ramani nzima ya mpango aliousuka. Dili likakubali. Hawa Waturuki pia wakaleta jamaa zao Waholanzi wakaunganisha nguvu na resources.

Yaw akaingia Ghana akakodi jengo kubwa lilolopo barabarani kabisa. Akajenga mlingoti kisha akaning'iniza bendera ya Marekani. Material aliyotumia inafikirisha sana - ukiwa mbali ni bendera ya Marekani iliyopungua namba ya nyota _ kati ya zile nyota 50, na kadri unavyozidi kuisogelea rangi inafifia hadi mwisho ukiifikia inakuwa bendera ya Ghana.[​IMG]Jengo lililopeperushwa bendera ya marekani kwa miaka 10.

Yaw akawaomba waturuki wale watafute 1st grade fingerprint scanner. Yule mhandisi akapewa jukumu ya kutambua software systems zinazotumiwa na Ubalozi wa Marekani. Kisha Wakazinunua kutoka kampuni kubwa ya Marekani ya mitandao. Hivyo waliweza kung'amua processes zote zinazotumiwa na wafanyakazi wa Ubalozini (consular).

Nje ya jengo lile Yaw akafunga satellite 2 za usalama, na pia nje kidogo ya lile jengo akafungua duka dogo la kuuza nguo na viatu.

Wakakodi apartment za hali ya juu na kununua magari kadhaa ya kusafirisha abiria.

vyombo vya ulinzi, usalama na uhamiaji vilivyodhalilishwa

Mwaka 2006 mpango mzima unaanza kutekelezwa rasmi. Yaw na team yake wakaanza kuingia mavyuoni, mitaani, vijiweni, vijijini, mjini pamoja na nje ya balozi halisi ya Marekani na kuzungumza na Waghana waliotoswa visa ya kuingia Marekani.[​IMG] Ubaalozi halisi ya Marekani nchini Ghana.

Wote waliokubali mpango wa kina Yaw wakawasafirishwa hadi Accra karibu na ofisi yao, wakawapa hifadhi katika apartment walizokodi pamoja na chakula.

Kisha kila asubuhi walifatwa kutoka wanapoishi na kupelekwa ofisini, huko michakato ya kutengeneza visa bandia ilifanyika kwa ustadi wa juu sana.

Waliweza kufoji vyeti vyote kwa kiwango cha daraja la kwanza, kuanzia taarifa za kibenki, hati za umiliki wa mali, hati za kuzaliwa, vyeti vya daktari, barua za mialiko, barua feki za kupata kazi na admissions za chuo n.k.

Kwa umakini uliotukuka, visa ya kwanza ilitengenezwa, kisha mteja akalipiwa gharama zote za kuingia Marekani na team ya Yaw. Huyu alitolewa kama chambo kuthibitisha uhalisia wa visa hiyo. Baada ya masaa 26 ya safari, Yaw alikenua meno yote 32, pamoja na timu yake wakapiga mvinyo wa pamoja baada ya yule jamaa waliyemtoa chambo kupokelewa na kukaribishwa Marekani kwa visa yao waliyoipika jikoni.[​IMG]Sampuli tu ya visa ya Marekani.

Lengo la muda mrefu la Yaw lilionekana kutimia. Mamia kwa maelfu ya Waghana wakawa wanachongewa visa za kuingia US. Huduma yao ikashamiri hadi nchi za jirani kama Cote d'Voire, Togo na Nigeria. Baada ya muda kidogo nchi za mbali kama Kenya, S.A, India, Palestine, Cameroon n.k. nazo zikaanza kupatiwa huduma.

Wakaanza kujitangaza chinichini kupitia vipeperushi, billboards na magazeti ya udaku. Yaw na timu yake wakaanza kupiga pesa ndefu sana, wateja walimiminika si kawaida. Ilifika kipindi gharama zikapanda hadi kufikia $6000, watu bado walimwagika - walipiga pesa sana. Hakika idara ya Ulinzi (department of Defence) ilidhalilishwa kupita maelezo, tena na kijana wa kawaida kabisa, mbaya zaidi - hawakudhalilishwa kwa masaa kadhaa ama siku kadhaa, bali ndani ya miaka 10 na miezi kadhaa.

Marekani anaamka usingizini - Operation Spartan Vanguard.

Nov 15, 2015 idara ya uhamiaji inashtuka baada ya kugundua kua kuna idadi kubwa sana ya wananchi wa baadhi ya nchi wanapata vibali vya kuingia Marekani, ilhali nchi hizo awali hazikuwa na idadi kubwa ya wananchi wake wanaoingia Marekani.

Upelelezi unaanza... Idara ya ulinzi inatoa tamko la kusitisha kutoa visa kwa baadhi ya nchi kwa muda wa mwezi mmoja. Mshangao mkubwa unaibuka; balozi hazitoi visa, lakini kuna watu bado wanaingia Marekani kwa visa mpya kabisa zinazoonesha wamezitoa ubalozini.

Msako 'wa kufa mtu' unapigwa, wasafiri wote wenye visa mpya kutoka nchi ambazo Marekani ilisitisha kutoa visa zao wanaanza kupelelezwa (interrogated). Pole pole wakaanza kukusanya taarifa, hadi wakafika conclusion kuwa kuna wahuni Ghana ndio wamesababisha fedheha hiyo kwa nchi kubwa yenye ulinzi wa hali ya juu zaidi.

Uvamizi katika ubalozi bandia wa Marekani - Vyombo vya usalama vya Marekani vilitambua fika kua Yaw na timu yake hadi kuweza kufanikisha zoezi la kuidhalilisha Marekani, walijipanga sana. Hivyo, hata wao walibidi 'wajikoki' haswa wasijekudhalilika tena. Zoezi zima la uvamizi halikuwa la 'kispoti spoti'.

Uvamizi huo ulipewa jina la 'Operation Spartan Vanguard'. Kiufupi, operation 'spartans' zote huanzishwa na Marekani kwenye mashambulizi ambayo vikosi vya usalama vimeshindwa kabisa kupata taarifa za awali juu ya eneo wanalopanga kushambulia, hivyo wanajipanga vizuri sana na kwa tahadhari ya juu kwakuwa wameshindwa kumsoma vizuri adui yao. Mara nyingi operatins hizi hazinaga mwisho mzuri. Mfano ni :- Operation Spartan Shield, Operation Spartan Strike, Operation Spartan Fury, Operation Spartan Jordan n.k.[​IMG] Wanajeshi katika 1 ya operation spartan.

Kikosi cha maangamizi kilishiba haswa, hawakufahamu kuwa adui zao ni watu 'walaini'. Kikosi kiliundwa na askari wa Ubalozi wa Marekani, maafisa wa polisi wa Ghana wenye mafunzo ya kijeshi ya Marekani, Taasisi ya upelelezi ya Ghana (Ghana detective bureau), kikosi cha kimataifa maalumu kwa kupamba na uhalifu, askari wa Ubalozi wa Canada, Askari wa uhamiaji wa Marekani pamoja na INTERPOL.

Tena na tena kwa mara nyingine Marekani anadhalilishwa, dunia nzima inamkodolea macho. Kina Yaw wanaisambaratisha Marekani kiulaini kabisa.

Yaw pamoja na timu yake wakiwa ndani ya ofisi yao, tayari walielewa mchezo mzima uliokuwa unaendelea, hawakuwa na papara, hawakuhutaji kujaza risasi kwenye magazine zao. Waliweza kutazama movie nzima wakivamiwa 'mubashara' (live) kupitia satellite mbili walizotegesha nje ya jengo lao.

■ Satellite ya kwanza ilionesha eneo la kuingia ndani ya ofisi yao. Hivyo adui asingeweza kuwafikia bila wao kumshtukia.

■ Satellite ya pili ilionesha usalama la eneo lao la siri la maficho.

Walivyoona wanavamiwa walimuita mmoja wa kijana wa kazi kisha wakampa kichupa, na kumuagiza akifungue kisha akitupe kwenye 'dustbin' ambayo ilikua mlango wa kuingilia. Kichupa hiko kilikuwa ni 'lachrymation spray' - hii ni chemikali kali sana yenye kusababisha muwasho mkali mno sehemu za wazi za mwili (macho, masikio, pua, skin pores, na yale mashimo mengine ya ndani ya c.hupi).[​IMG]askari wa Spartan vanguard wakihenyeshwa.

Baada ya hapo Yaw na team yake wakatoroka kupitia 'built in tunnels' - mifereji ya ndani, ambayo ilipita chini kwa chini na kutokea kwenye lile duka la nguo na viatu nje ya ofisi yao. - Baada ya hapo lazima waingie bar kupongezana .

Kikosi kazi kile cha Wamarekani kiliambulia muwasho 'wa upupu' na kuwakamata baadhi ya wafanyakazi ambao wala hawakuelewa shughuli haramu ziliyokuwa zikiendelea mule ndani.

Upelelezi bado unaendelea, hadi leo kiongozi mkuu wa shambulizi la Spartan vanguard hajaeleza kupatikana kwa wahalifu wakuu na dau nono tayari limetangazwa kwa atakayefanikiwa kukamatwa kina Yaw.

Katika uvamizi huo vitu kadhaa vilipatikana vikiwemo passport 190 (kutoka nchi 10 tofauti), printer 5 za kisasa, HD camera, mihuri bandia 75, laptop 8, smartphones pamoja na documents zinginge nyingi.[​IMG]baadhi ya vitu vilivyopakipatikana
[​IMG]

Kinachowaliza zaidi taasisi za usalama za Marekani

Wizara ya ulinzi, kitengo cha uhamiaji na maafisa wa usalama wa Marekani wameshindwa kabisa kung'amua mafumbo yafuatayo;-

○Wahuni wa Ghana wenye teknolojia ya kawaida kabisa wamewezaje kukamilisha zoezi 'sensitive' kama hilo kwa zaidi ya muongo mzima?!

○Wameshindwa kung'amua ni visa ya daraja gani ilikuwa inatengenezwa na wahuni hao?!

○Wameshindwa kabisa kung'amua utofauti kati ya visa halali na visa bandia.

○Wameshindwa kung'amua idadi kamili ya watu walipewa visa hizo, wangapi walirudi nchini kwao na wangapi bado wanaishi Marekani.

○Wameshindwa kung'amua jinsi gani wataweza kuwatambua na kuwakamata waliokabidhiwa visa bandia na kuingia Marekani.

○Watawezaje kumzuia Yaw na team yake kuendelea kuchapisha visa hizo bandia. Vipi kama wakiunganisha nguvu na maadui wao wakubwa?!

○Wameshindwa kabisa kupata 'identity' kamili ya Yaw na team yake. (Kwa kifupi jina la Yaw ni la kufikirika tu - uchunguzi unaendelea).

○Je ni kivipi wataweza kujisafisha na fedheha hiyo katika dunia paba ya kiintelijensia - watawezaje kuficha udhaifu wao??

My take

Wakati dunia nzima ikiiheshimu na kuisujudia marekani katika swala la ulinzi na usalama, bado naamini kuna vitu vingi vinahitaji kuwa 'fixed'. Nakubali Jeshi lao ni pana sana, lina maaskari wengi na wenye uwezo na fitness nzuri, wamewekeza pesa ndefu, wana miundombinu, vifaa, mbinu na teknolojia za hali ya juu, lakini akitokea mtu mmoja tu mwenye nia thabiti, anaweza 'kuwachambua kama karanga', kuwageuza kama chapati na kiwadhalilisha kwa kadri atakavyo machoni mwa kila mtu, tena mchana kweupeee.

-Meanwhile nafuatilia mubashara uzi wa mkuu The bold jinsi Usama bin Laden alivyowashikisha ukuta Wamarekani.

Baadhi ya taarifa nimepakua kutoka Source mbali mbali za internet zikiwemo:-
BBC News How did fake US embassy operate in Ghana for a decade? - BBC News
US Department of staste Regional Security Office Ghana Shuts Down "Fake Embassy"
BBC focus on Africa BBC World Service - Focus on Africa, 04/12/2016 GMT
The Washington post Mobsters ran a fake U.S. Embassy in Ghana for 10 years, flying the flag and issuing visas for $6,000
Pamoja na source zingine nyingi.

Jumanne, 28 Februari 2017

mwalimu ajinyonga singida


  1. Shule ya Sekondari Tumuli katika Wilaya ya Mkalama, mkoani Singida, Richard Makala (58) amejinyonga kwa kamba kutokana na kile kinachodhaniwa kuelemewa na upweke.

    Kamanda wa Polisi Mkoa wa Singida, Debora Magiligimba, amesema mjini Singida kuwa, Makala alijinyonga jana saa 1 asubuhi.


    Ameeleza kuwa Makala alikutwa amejinyonga kwa kutumia kamba iliyotengenezwa kwa vipande vya chandarua iliyofungwa juu ya mti umbali wa mita 130 kutoka nyumbani kwake.

    Amesema, chanzo cha tukio hilo hakijajulikana na kwamba hakuna mtu au watu wanaoshikiliwa kutokana na tukio hilo na kuongeza kuwa polisi inaendelea na upelelezi kubaini kilichomsibu mwalimu huyo.

    Hata hivyo, Mjumbe wa Bodi ya shule hiyo, Mabruki Ng’ui amelisema mwalimu huyo alikuwa anaishi peke yake kwa muda mrefu baada ya mkewe ambaye ni Mchungaji wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania Tanzania (KKKT) Kitusha wilayani Iramba kuamua kutengana naye kutokana na unywaji pombe.

    "Huyu bwana amekuwa kwenye ndoa ya jina tu maana mke wake amekuwa akiishi mbali naye kwa kipindi kirefu sana, amekuwa mpweke kwa muda mrefu mno huenda hicho ndicho kilichosababisha ajitoe roho yake," amesema Mjumbe huyo wa Bodi.

    Makala ni mzaliwa wa kijiji cha Ndago, wilayani Iramba na anatarajiwa kuzikwa leo nyumbani kwake.

    Ameacha mjane na watoto watano.


ona hii makonda akiombewa duwa na waislamu

Mkuu wa mkoa wa Dar Es Salaam,mheshimiwa Paul Makonda,ameombewa duwa na waislamu kama
baraka na kinga kutoka kwa viongozi mbalimbali wa dini ya kiislamu katika ufunguzi wa mashindan
ya kusoma Quran nchini.Dua hyo aliipata kutoka kwa viongozi wenye elimu kubwa ya dini
ya kiislamu nchini

Jumanne, 31 Januari 2017

MATOKEO KIDATO CHA NNE 2016

http://matokeoyamitihani.blogspot.com/2016/01/csee-form-four-examination-results.html

MATOKEO YA KIDATO CHA NNE KUONYESHA KIWANGO CHA UFAULU WA WANAFUNZI KUPANDA,KATIKA MATOKEO HAYO WAVULANA WANAONGOZA KWA ASILIMIA NYINGI UKILINGANISHA NA WASICHANA,WAZIRI WA ELIMU NA MAFUNZO NYA UFUNDI PROFESA JOYCE NDALICHAKO,AMESEMA KUWA UFAULU HUO UMEPANDA KUTOKANA NA JUHUDI MBALI MBALI ZILIZOWEKWA NA SERIKALI YYAMETANGAZWA LEO NA A AWAMU YA TANO CHINI YA RAISI, JOHN POMBE MAGUFULI,KUYAONA INGIA KWENYE LINK HAPO CHINI,JUU

Jumapili, 29 Januari 2017

AJALI MBAYA YA TRENI YATOKEA
             Ajali mbaya  ya treni imetokea maeneo ya jirani na mto ruvu yakihusisha treni iliyokuwa inatokea kigoma kwenda dar es salaam.mpaka sasa bado haijathibishwa ni watu wangapi wamefariki au kujeruhiwa ,na mpka tunapokea taarifa hii hakuna watu wa msaadsa kama vile polisi na ambulance waliofika katika eneo la tukio.Tunajitahidi kuwaletea pich na hata video lza tukio husika soonImage result for ajali ya treni ruvu

Jumatatu, 9 Mei 2016

nafasi za kazi

Job Opportunity- Financial Controller, Application Deadline: 14 May 2016

VACANCY
Our Client; is a private liability Pan- African Company with headquarters in Dar es salaam,Tanzania.The company provides a comprehensive range of products and services relating to water treatment chemicals,weste water treatment,water meters,valves,pipes,water pumps,fittings,agriculture,and composite manhole covers. Hurry and send your cv viarecruitment@jobconnect.co.tz before 14th May,2016.

Job Description:
Department: Finance
Job Title: Financial Controller
Duty station: Dar es Salaam
Immediate Supervisor:  Managing Director

General Position Summary: The Financial Controller oversees the day to day activities of the finance team, monitor the accounting and finance departments' policies and procedures, set budgets, provide guidance on complex tax and compliance issues, contribute to the financial strategy discussions at the company and maintains a sound accounting and financial management system in accordance with Junaco Tanzania rules and regulations.

Detailed Responsibilities:-
Accounting:

You are responsible for ensuring that all accounting allocations are appropriately made and documented. May also perform cash management functions and oversee accounts payable, accounts receivable, cash disbursements, Payroll and bank reconciliation functions. 
Internal Controls:

You are responsible for establishing and executing internal controls over the company’s accounting and financial procedures. This includes reviewing and approving all invoices to be paid, as well as reviewing accounts receivable aging reports. You are also responsible for coordinating with external tax accountants for income tax preparation and auditors who prepare internal audits of the company. This includes keeping company records organized and readily available for audit.
Financial Planning and Reporting:

You are responsible for all banking and finance activities. This includes negotiating lines of credit and vendor agreements, as well as reviewing all financial contracts, financing agreements and insurance policies. Responsible for providing accurate and comprehensive financial information to Managing Director for long-term financial strategizing. You will be required to fulfill this responsibility as well; in any case, you must provide crucial financial data and work with executive management to coordinate all financial planning functions with business operations. 
Financial Analysis:

In addition to financial reporting, you must be skilled at in-depth financial analysis and providing expert financial perspective and opinions. Must be proficient in spreadsheet design that is often complex. While MD is responsible for finalizing financial policy, your financial analysis skills are instrumental in helping to assess risk, analyze efficiency and inform policy decisions made by the board management.
Daily duties include:

Management of the finance function and overseeing or supervise the finance team.Preparation of budgets, forecasts and cash flowsMaintenance of financial ledgers and accounting processesPreparation of Monthly Consolidated P&L and Balance SheetTimely production of statutory and internal financial reportsPreparation of letter of credits (LC’s) to clients and suppliersCash management and treasury dutiesEnsuring that appropriate systems and internal controls are implemented and maintainedOverseeing the Payroll processPreparation of VAT returns
Other duties:

Carry out other duties that may from time to time be assigned to you by the managing director. 
Preferred Skills required:

A formal accounting education and membership with any accounting bodyCommercial enterprise managerial reporting experience is mustGood ability to motivate, develop and manage team and efficiency to work with other similar staffTechnical and functional skills in financial controllingResilient Customer focus and strong analytical and financial skillsGood Communication skills and exhibit excellent professional ethics

Education level:
A Bachelor degree in Accountancy,or commerce,equivalent from recognized university/ institution
Possession of post graduate degree, CPA
At least five (5) years experience in senior management position
Able to use effectively computerized integrated financial Management System (Palladium system)

Position to be stationed: DAR-ES-SALAAM
Age: 35 Above
Type of Job:  Permanent
Working hours /days: 6-Full days and Saturday half day.
Remuneration:
Salary: 5,000,000/=
Lunch at the office
Medical cover
Transport allowance of 100,000 monthly
Number of References Required: 3
Deadline is 14th May, 2016.
Only short-listed candidates w

Jumapili, 8 Mei 2016

mtoto asiye na mkono shinda tuzo ya mtu mwenye mwandiko bora duniani

ImageMsichana asiye na mikono ashinda shindano la muandiko bora Marekani

Msichana wa miaka saba aliyezaliwa bila mikono ameshinda shindano la muandiko mzuri nchini Marekani.

Anaya Ellick kutoka Chesapeake,Virginia hatumii viungo vya kumsaidia wakati anapoandika.

Wakati anapoandika yeye husimama huku akishikilia kalamu yake katika mikono.

Mwalimu wake mkuu Tracy Cox kutoka shule ya Greenbrier Christian amemtaja kuwa mtu wa mfano mwema.

''Yeye uhakikisha kuwa hakuna kitu kinachomzuia kufanya atakalo'',alisema Cox.''Ni mkakamavu na ana muandiko mzuri katika darasa lake''.

Msichana huyo anadaiwa kuwashinda washindani wengine 50 ili kushinda taji hilo la kitaifa.

Orodha hiyo ya tuzo huwazawadi wanafunzi wenye akili, matatizo ya kimwili, au ulemavu endelevu.

Jumamosi, 7 Mei 2016

London yaandika historia mpya

Jiji la london leo limeandika historia mpya kwa kumpata meya wa kwwanza muislamu.Bwana Sadiq khan ambaye ni muingereza mwenye asili ya Pakistan
amefanikiwa kuchukua kiti hicho cha umeya kwa asilimia 56.5 dhidi ya mpinzani wake mkubwa bwana Troy Zac
ambaye alijipatia asilimia 43. 2 ya kura zote. Sadiq Khan baada ya kutangazwa kwa matokeo aliyasema haya"mtu kama mimi kuchaguliwa kuwa meya wa london sikuwahi kufikiria kwa kweli naahidi kuwa meya wa watu wote wa london

Ijumaa, 6 Mei 2016

BREAKING: UKAWA wametangaza maamuzi yao, sababu Bunge halionyeshwi live kwenye TV

Utaratibu mpya ni wa timu maalum iliyopewa kazi maalum ya kurekodi matukio ya Bunge yote yanayofaa kufikishiwa Wananchi na hayo matukio ndio wanapewa Waandishi wa habari ila hakuna tena utaratibu kama wa zamani kwamba kila mwandishi anaweza kurekodi kwa Camera yake chochote anachoona ni habari.
April 22 2016 vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA) wametangaza kutokuchangia bajeti zote zinazoendelea ndani ya bunge hadi pale Serikali itakaporekebisha vipengele vinavyo bana uhuru wa bunge kama vile kuruhusu urushwaji wa matangazo ya moja kwa moja na vyombo vingine kurekodi bila vizuizi.http://www.ippmedia.com/media/picture/large/Mbowe-28Feb2015.jpg

Ads Inside Post