Alhamisi, 15 Desemba 2016

ifahamu kensa

*Dr. Brian Berry wa Marekani amegundua kensa mpya kwa binadamu inayosababishwa na Silver Nitro Oxide. Unaponunua kadi ya simu usiichune kwa kucha kwani imo hiyo Silver Nitro Oxide na inaweza kusababisha kensa ya ngozi. Watumie ujumbe huu wale uwapendao.*

*Nukuu muhimu za afya*
*��sikiliza simu kwa sikio la kushoto.*
*��usimeze dawa na maji baridi*
*��usile chakula kizito baada ya saa kumi na moja jioni.*
*��kunywa maji mengi asubuhi na kidogo usiku.*
*��wakati mzuri wa kulala ni kuanzia saa nne hadi kumi usiku.*
*��usilale mara baada ya kula dawa au chakula.*
*��ikiwa charge imebakia kijino cha mwisho usipokee* *simu kwani mionzi inakuwa na nguvu kwa mara 1000 zaidi.*
*��unaweza kuwatumia haya wale unaowajali?*
*Mie nimeshafanya.*
*Huruma haigharimu kitu lakini elimu ni nuru.*
*������ MUHIMU ������*
*Jumuiya ya uchunguzi ya marekani imetoa majibu mapya. Usinywe chai kwenye vikombe vya plastic. Na usile Chochote kwenye mifuko ya plastic. Plastic ikikutana na joto inatoa vitu vinavyo sababisha aina 52 za kensa.

uke kutka harufu mbaya

UKE KUTOA HARUFU MBAYA

  

Leo ningependa tuzungumzie tatizo la uke kutoa harufu mbaya, kwani ni tatizo ambalo linawaathiri dada zetu sana, na huwafanya wasiwe na uhuru wanapokuwa faragha na wapenzi wao, na kuwafanya wasiwe na raha, na kupoteza kujiamini.
Tatizo la kutoa harufu ukeni husababishwa na sababu kadhaa Kama ifuatavyo.

1.Bacterial vaginosis
Kwa kawaida, uke huwa na bakteria ambao huitwa lactobacilli, bakteria hawa ni wazuri na hawamletei shida yeyote mwanamke, bakteria hawa huulinda uke usishambuliwe na bakteria wabaya ambao ndio husababisha magonjwa. Kinachowawezesha bakteria hawa waweze kukaa kwenye uke ni hali ya utindikali wa uke(vaginal acidity); hali hii ya utindikali wa uke inapobadilika na kupungua kwa sababu yeyote ile, husababisha bakteria hawa kupungua, na hivyo kutoa nafasi kwa bakteria wabaya kukua kwa wingi, na kushambulia afya ya uke, hivyo kusababisha harufu(harufu hii hutokana na uchafu unaotengenezwa na bakteria hawa).Hali hii kitaalamu ndio huitwa bacterial vaginosis.Ni muhimu kufahamu kuwa ugonjwa huu hauambukizwi kwa njia ya zinaa, japokuwa wanawake ambao wanajihusisha katika ngono wanakuwa katika hatari kubwa zaidi ya kpata ugonjwa huu, pia wanwake wanaofanya “douching”(kujisafisha ukeni kwa kuingiza kidole) na wanaoshiriki mapenzi kinyume cha maumbile wako kwenye uwezekano mkubwa wa kupata bacterial vaginosis.

2.Magonjwa ya zinaa (Sexually transmitted diseases;Vaginal Trichomoniasis, gonorrhea,chlamydia)
Ugonjwa wa zinaa unaoitwa kitaalamu vaginal trichomoniasis ndio ugonjwa wa zinaa ambao unaathiri wanawake wengi zaidi kuliko ugonjwa mwingine wowote wa zinaa. Ugonjwa huu unasababishwa na protozoa anaejulikana kwa jina la Trichomona vaginalis. Na huambukizwa kwa njia ya ngono. Dalili za ugonjwa huu kwa wanawake ni kutoa majimaji yanayotoa harufu kali, yenye rangi ya njano–kijani,kuwashwa ukeni.
Gonorrrhea kwa kawaida pia huweza kusababisha kutokwa na majimaji yenye harufu ukeni, na kuwashwa, maumivu wakati wa kukojoa, maumivu wakati wa kufanya mapenzi, na maumivu chini ya kitovu (japokuwa, kwa gonorhea wanawake wengi wanaweza wasionyeshe dalili yoyote kwa muda mrefu).
Mara nyingi, inaweza kuwa vigumu kwa daktari kuweza kutofautisha baina ya magonjwa haya ya zinaa (hasa kwa mazingira yetu duni); Hivyo basi mara nyingi daktari atatoa dawa kwa ajili ya magonjwa haya matatu ya zinaa pale anapofikiri kuwa mgonjwa wake ana tatizo la ugonjwa wa zinaa.

3.Fangasi za ukeni (Vagina candidiasis)
Fangasi za ukeni pia huweza kusababisha kutokwa na harufu kali ukeni, japokuwa si kwa kiwango kikubwa sana kama sababu mbili hapo juu. Pia, mara nyingi mwanamke mwenye tatizo la fangasi za ukeni atalalamika kuhusu kuwashwa zaidi kuliko harufu.
Dalili za fangasi za ukeni ni pamoja na kutoa majimaji mazito ya rangi nyeupe (kama maziwa mtindi) yenye harufu, kuwashwa ukeni,pamoja na kusikia maumivu wakati wa kufanya mapenzi.
Vitu ambavyo vinamuweka mwanamke katika hatari ya kupata fangasi za ukeni ni pamoja na kufanya “douching” (kujisafisha uke kwa kuingiza kidole), kuvaa nguo za kubana, kuvaa nguo za ndani ambazo sio za cotton, kuvaa nguo za ndani ambazo hazijapigwa na jua/kupigwa pasi, usafi hafifu wa sehemu za siri, matumizi ya vyoo vya kukaa na matumizi ya dawa za uzazi wa mpango.

Je, nini cha kufanya ili kujiepusha na harufu mbaya ya sehemu za siri kwa mdada?
-Epuka kusafisha uke kwa kuingiza kidole ukeni-Uke usafishwe kwa maji ya vuguvugu na sabuni ya kawaida ya kuogea (sio medicated soap), bila kuingiza kidole au kitu chochote ndani ya uke
-Epuka matumizi ya madawa ya antibiotics kwa muda mrefu bila ya kuambiwa na daktari-kwani dawa hizi zikitumika kwa muda mrefu na bila ushauri wa daktari husababisha mabadiliko katika bakteria wa kwenye uke na kupelekea magonjwa na harufu mbaya
-Vaa nguo za ndani za cotton
-Epuka nguo za kubana sana mwili
-Nguo ya ndani ianikwe nje; sehemu ambayo itapigwa na jua (na sio ndani ya chumba); au nguo za ndani zipigwe pasi kabla ya kuvaliwa,
-Unapokuwa kwenye siku zako zingatia usafi na kubadilisha pedi kama inavyotakiwa(mara 2-3 kwa siku)
-Epuka kutumia vyoo vya umma ambavyo ni vya kukaa,
-Jikinge na magonjwa ya zinaa,
-Epuka kuvaa nguo nyingi na/au nzito wakati wa kulala; vaa nguo nyepesi ambayo itaruhusu uke kupata hewa ya kutosha.
-Jisafishe vizuri kila baada ya kumaliza haja ndogo,
-Kitu kingine ambacho ni muhimu sana kufahamu, ikitokea ukaona kuwa uke wako unatoa harufu, kuuosha kwa maji mengi na sabuni nyingi mara nyingi, sio suluhisho bali unazidi kuleta matatizo zaidi kwa sababu unazidi kupunguza idadi ya bakteria wazuri, na kubadilisha hali ya utindikali wa uke na hivyo kukaribisha bakteria wabaya kwa wingi zaidi!!
-Na kitu cha mwisho ambacho ni muhimu zaidi, ni kwetu wanaume, unapoona mwenzi wako ana tatizo hili, usimseme vibaya au kumkaripia au kumtukana; Unatakiwa kutambua kuwa huo ni ugonjwa na umsaidie kuweza kuonana na wataalamu wa tiba kwa

Alhamisi, 12 Mei 2016

fahamu nchi zinazoongiza kwa ufisadi afrika

ImageWaziri mkuu wa Uingereza David Cameron alinaswa na kamera akiidunisha Nigeria kuwa mafisadi wakuu duniani

Baada ya waziri mkuu wa Uingereza David Cameron kunaswa na kamera akiidunisha Nigeria kuwa mafisadi wakuu kote duniani BBC imeamua kuangazia kwa umakini ikiwa matamshi hayo ni ya kweli.

Je Nigeria imeorodheshwa katika nafasi ipi katika orodha ya mataifa fisadi kwa mujibu wa shirikisho la kupambana dhidi ya ufisadi duniani Transparency International ?

ImageTanzania inaorodheshwa katika nafasi ya 117 duniani

Ni vigumu kuelezea kwa kina ama hata kupiga msasa ufisadi katika mataifa kwani kila mwanauchumi anaelezea ufisadi akitumia mizani tofauti na mwenziye.

Kwa sababu hiyo tutatumia orodha ya mwaka wa 2015 ya shirikisho la kupambana dhidi ya ufisadi, Transparency International, ili kukupa taswira ya mataifa ya kanda ya Afrika Mashariki na jinsi yanavyolinganishwa na mataifa mengine duniani katika mizani ya ubadhirifu na wizi wa mali ya uma.

Cha mno hata hivyo sharti tuweke bayana kuwa Nigeria sio taifa fisadi zaidi duniani.

ImageImageNigeria imeorodheshwa katika nafasi ya 136 Nigeria kati ya mataifa 167.

Nigeria imeorodheshwa katika nafasi ya 136 Nigeria kati ya mataifa 167.

Kenya kwa mfano inasemekana kuwa na ufisadi mkubwa hata kuishinda Nigeria.

ImageAPImageZimbabwe wanaorodheshwa katika nafasi ya 150 duniani kwa ufisadi.

Katika kanda ya Afrika Mashariki , mali ya umma inafujwa sana na viongozi wa serikali hali ambayo inaiweka mataifa ya kanda katika nafasi za mwisho mwisho kuashiria viwango vya juu vya ufisadi.

Kati ya mataifa kumi Fisadi zaidi duniani Somalia inaongoza ikifwatwa na Sudan ,Sudan Kusini, Eritrea, Burundi, DRC, Uganda, Kenya Tanzania Ethiopia na kisha Rwanda katika usanjari huo.

Somalia inaongoza kwa Ufisadi duniani katika nafasi ya 167.

Viwango vya ufisadi vinanasibishwa na Korea Kaskazini.

Nchi iliyojitenga kabisa na ufisadi kanda ya Afrika Mashariki na kati ni Rwanda.

ImageRwanda inaorodheshwa katika nafasi ya 44 duniani.

Taifa hilo linaloongozwa na rais Paul Kagame linaorodheshwa katika nafasi ya 44 duniani.

Je unakumbuka rais Robert Mugabe aliyewadunisha wakenya kwa kuwa wezi ?

Kulingana na orodha hii iliyotayarishwa na shirika la TI Zimbabwe wanaorodheshwa katika nafasi ya 150 duniani kwa ufisadi.

Wanagawana nafasi hiyo na Burundi.

Orodha ya mataifa 10 fisadi zaidi kanda ya Afrika Mashariki na Duniani.

1. 167 Somalia / Korea Kaskazini

2. 165 Sudan

3. 163 South Sudan/ Angola

4. 154 Eritrea/Yemen / Turkmenistan / Syria

5. 150 Burundi / Zimbabwe

6. 147 Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo / Chad / Myanmar /

7. 139 Kenya / Uganda

8. 117 Tanzania

9. 103 Ethiopia

10. 44 Rwanda

Jumatano, 11 Mei 2016

msanii wa bongo movies afariki dunia

May 12 2016 ripoti zilianza kusambaa kwenye mitandao ya kijamii kwa baadhi ya mastaa wa filamu na Muziki nchini, kuhusiana nataarifa ya kufariki kwa mmoja kati ya wachekeshaji maarufu nchini Tanzania,  Mohammed Abdallah  (Kinyambe) kutoka kwenye maigizo ya Vituko Show.

walimu walipwa kuku badala ya mshahara

ImageAFPImageWalimu walipwa kuku kama mshahara

Mji mmoja nchini Uzbekistan umekua ukiwapa waalimu wake kuku kama mshahara badala ya pesa. Mamlaka za mji wa Nukus katika jimbo linalojitawala la Karakalpakstan wamekua wakitia vifaranga wachanga kwa walimu kutokana na uhaba wa pesa nchini humo.

Kituo cha radio kinachofadhiliwa na Marekani{Radio Ozodlik} kimemnukuu mwalimu mmoja akilaani hatua hiyo kama aibu kubwa kwa mamlaka.

Mwalimu huyo aliyeghadhabishwa na hatua hiyo amesema hataki vifaranga kwa sababu anaweza kuwapata sokoni, lakini wanataka pesa zao.

Vifaranga wanaotolewa kama mshahara wana gharama ya dola mbili kila mmoja, ikiwa ni maradufu bei inayouzwa vifaranga sokoni.

Mamlaka za Uzbekistan hazikubalii uhuru wa vyombo vya habari na raia wa huko hutegemea vyombo vya habari vya kimataifa kutoa sauti yao, ila hawajitambulishi.

Uzbekistan imekumbwa na uhaba wa fedha kwa miaka sasa hali inayosababisha serikali kuchelewesha mishahara ya wafanyikazi na malipo ya uzeeni.

Mapema mwezi huu wafanyikazi wa serikali katika mji mkuu,Tashkent walilalamikia kwamba hawakuwa wamelipwa mshahara kwa miezi miwili kwa sababu benki hazikuwa na pesa.

justin bieber sitapiga picha tena na mashabiki

ImageJustin Bieber asema hatopiga picha tena na mashabiki wake

Iwapo hujagundua basi ujue kwamba nyota wa muziki wa Pop Justin Bieber yuko katika ziara ya ulimwengu.

Kwa sasa yuko nchini Marekani ambapo alionekana amepumzika katika mbuga moja kabla ya tamasha yake mjini Boston.

ImageBieber alivyoandika katika mtandao wa instagram

Bieber ambaye alikuwa hana viatu aliwavutia mashabiki lakini akakataa kuzungumza nao hadi watakapoweka simu zao chini.

Haijulikani iwapo picha alizochukua na mashabiki wake katika lango la mbuga hiyo zilikuwa za mwisho,lakini baadaye jioni alichapisha katika mtandao wake wa Instagram kwamba hatapiga picha tena na mashabiki.

ImageHivi ndivyo mashabiki wake walivyomjibu

''Iwapo utakutana nami mahali ujue kwamba sitapiga picha tena'',aliandika.

Alielezea vile watu hawaezi hata kumsalimia ama kujua kwamba hata yeye ni binaadamu na hivyobasi kumfanya kujihisi kama mnyama na sasa anataka kuheshimiwa.

ImageTWITTERImageJustin Bieber aiwa nchini Marekani

Aliongezea: Najua kwamba watu hawatafurahia lakini hakuna mtu anayenidai picha.

waziri mkuu atimuliwa bungeni

ImageGETTYImageWaziri mkuu wa New Zealand

Waziri Mkuu mpya wa New Zealand John Key ametupwa nje ya bunge na spika baada ya kukaidi kufuata kanuni za bunge.

Bunge hilo limekua na mjadala mkali kuhusu sakata ya akaunti za siri ambazo zinadaiwa kuwepo kisiwa cha Panama.

Spika wa Bunge David Carter ametetea hatua yake na kusema Waziri Mkuu alikaidi onyo la kutoheshimu kanuni za bunge, na hivyo hakua na kinga ila kumuadhibu, kama wabunge wengine.

Rekodi za bunge zimenakili kwamba Waziri Mkuu huyo aliwahi kutupwa nje ya bunge mara tatu wakati akiwa mbunge.

Hata hivyo si mara ya kwanza Waziri MKuu NewZealand anatupwa nje ya bunge.

Waziri Mkuu wa zamani Helen Clark alitupwa nje mwaka 2005 huku naye mtangulizi wake, David Lange akijipata pabaya miaka ya 1986 na 1987.

Ads Inside Post