UDAKU WA TOWN

Alhamisi, 15 Desemba 2016

ifahamu kensa

*Dr. Brian Berry wa Marekani amegundua kensa mpya kwa binadamu inayosababishwa na Silver Nitro Oxide. Unaponunua kadi ya simu usiichune kwa kucha kwani imo hiyo Silver Nitro Oxide na inaweza kusababisha kensa ya ngozi. Watumie ujumbe huu wale uwapendao.*

*Nukuu muhimu za afya*
*��sikiliza simu kwa sikio la kushoto.*
*��usimeze dawa na maji baridi*
*��usile chakula kizito baada ya saa kumi na moja jioni.*
*��kunywa maji mengi asubuhi na kidogo usiku.*
*��wakati mzuri wa kulala ni kuanzia saa nne hadi kumi usiku.*
*��usilale mara baada ya kula dawa au chakula.*
*��ikiwa charge imebakia kijino cha mwisho usipokee* *simu kwani mionzi inakuwa na nguvu kwa mara 1000 zaidi.*
*��unaweza kuwatumia haya wale unaowajali?*
*Mie nimeshafanya.*
*Huruma haigharimu kitu lakini elimu ni nuru.*
*������ MUHIMU ������*
*Jumuiya ya uchunguzi ya marekani imetoa majibu mapya. Usinywe chai kwenye vikombe vya plastic. Na usile Chochote kwenye mifuko ya plastic. Plastic ikikutana na joto inatoa vitu vinavyo sababisha aina 52 za kensa.

Imechapishwa na jerry kwa 20:57 Hakuna maoni:
Tuma Hii kwa Barua pepeBlogu Hii!Chapisha kwenye XShiriki kwenye FacebookShiriki kwenye Pinterest
Lebo: habari

uke kutka harufu mbaya

UKE KUTOA HARUFU MBAYA

  

Leo ningependa tuzungumzie tatizo la uke kutoa harufu mbaya, kwani ni tatizo ambalo linawaathiri dada zetu sana, na huwafanya wasiwe na uhuru wanapokuwa faragha na wapenzi wao, na kuwafanya wasiwe na raha, na kupoteza kujiamini.
Tatizo la kutoa harufu ukeni husababishwa na sababu kadhaa Kama ifuatavyo.

1.Bacterial vaginosis
Kwa kawaida, uke huwa na bakteria ambao huitwa lactobacilli, bakteria hawa ni wazuri na hawamletei shida yeyote mwanamke, bakteria hawa huulinda uke usishambuliwe na bakteria wabaya ambao ndio husababisha magonjwa. Kinachowawezesha bakteria hawa waweze kukaa kwenye uke ni hali ya utindikali wa uke(vaginal acidity); hali hii ya utindikali wa uke inapobadilika na kupungua kwa sababu yeyote ile, husababisha bakteria hawa kupungua, na hivyo kutoa nafasi kwa bakteria wabaya kukua kwa wingi, na kushambulia afya ya uke, hivyo kusababisha harufu(harufu hii hutokana na uchafu unaotengenezwa na bakteria hawa).Hali hii kitaalamu ndio huitwa bacterial vaginosis.Ni muhimu kufahamu kuwa ugonjwa huu hauambukizwi kwa njia ya zinaa, japokuwa wanawake ambao wanajihusisha katika ngono wanakuwa katika hatari kubwa zaidi ya kpata ugonjwa huu, pia wanwake wanaofanya “douching”(kujisafisha ukeni kwa kuingiza kidole) na wanaoshiriki mapenzi kinyume cha maumbile wako kwenye uwezekano mkubwa wa kupata bacterial vaginosis.

2.Magonjwa ya zinaa (Sexually transmitted diseases;Vaginal Trichomoniasis, gonorrhea,chlamydia)
Ugonjwa wa zinaa unaoitwa kitaalamu vaginal trichomoniasis ndio ugonjwa wa zinaa ambao unaathiri wanawake wengi zaidi kuliko ugonjwa mwingine wowote wa zinaa. Ugonjwa huu unasababishwa na protozoa anaejulikana kwa jina la Trichomona vaginalis. Na huambukizwa kwa njia ya ngono. Dalili za ugonjwa huu kwa wanawake ni kutoa majimaji yanayotoa harufu kali, yenye rangi ya njano–kijani,kuwashwa ukeni.
Gonorrrhea kwa kawaida pia huweza kusababisha kutokwa na majimaji yenye harufu ukeni, na kuwashwa, maumivu wakati wa kukojoa, maumivu wakati wa kufanya mapenzi, na maumivu chini ya kitovu (japokuwa, kwa gonorhea wanawake wengi wanaweza wasionyeshe dalili yoyote kwa muda mrefu).
Mara nyingi, inaweza kuwa vigumu kwa daktari kuweza kutofautisha baina ya magonjwa haya ya zinaa (hasa kwa mazingira yetu duni); Hivyo basi mara nyingi daktari atatoa dawa kwa ajili ya magonjwa haya matatu ya zinaa pale anapofikiri kuwa mgonjwa wake ana tatizo la ugonjwa wa zinaa.

3.Fangasi za ukeni (Vagina candidiasis)
Fangasi za ukeni pia huweza kusababisha kutokwa na harufu kali ukeni, japokuwa si kwa kiwango kikubwa sana kama sababu mbili hapo juu. Pia, mara nyingi mwanamke mwenye tatizo la fangasi za ukeni atalalamika kuhusu kuwashwa zaidi kuliko harufu.
Dalili za fangasi za ukeni ni pamoja na kutoa majimaji mazito ya rangi nyeupe (kama maziwa mtindi) yenye harufu, kuwashwa ukeni,pamoja na kusikia maumivu wakati wa kufanya mapenzi.
Vitu ambavyo vinamuweka mwanamke katika hatari ya kupata fangasi za ukeni ni pamoja na kufanya “douching” (kujisafisha uke kwa kuingiza kidole), kuvaa nguo za kubana, kuvaa nguo za ndani ambazo sio za cotton, kuvaa nguo za ndani ambazo hazijapigwa na jua/kupigwa pasi, usafi hafifu wa sehemu za siri, matumizi ya vyoo vya kukaa na matumizi ya dawa za uzazi wa mpango.

Je, nini cha kufanya ili kujiepusha na harufu mbaya ya sehemu za siri kwa mdada?
-Epuka kusafisha uke kwa kuingiza kidole ukeni-Uke usafishwe kwa maji ya vuguvugu na sabuni ya kawaida ya kuogea (sio medicated soap), bila kuingiza kidole au kitu chochote ndani ya uke
-Epuka matumizi ya madawa ya antibiotics kwa muda mrefu bila ya kuambiwa na daktari-kwani dawa hizi zikitumika kwa muda mrefu na bila ushauri wa daktari husababisha mabadiliko katika bakteria wa kwenye uke na kupelekea magonjwa na harufu mbaya
-Vaa nguo za ndani za cotton
-Epuka nguo za kubana sana mwili
-Nguo ya ndani ianikwe nje; sehemu ambayo itapigwa na jua (na sio ndani ya chumba); au nguo za ndani zipigwe pasi kabla ya kuvaliwa,
-Unapokuwa kwenye siku zako zingatia usafi na kubadilisha pedi kama inavyotakiwa(mara 2-3 kwa siku)
-Epuka kutumia vyoo vya umma ambavyo ni vya kukaa,
-Jikinge na magonjwa ya zinaa,
-Epuka kuvaa nguo nyingi na/au nzito wakati wa kulala; vaa nguo nyepesi ambayo itaruhusu uke kupata hewa ya kutosha.
-Jisafishe vizuri kila baada ya kumaliza haja ndogo,
-Kitu kingine ambacho ni muhimu sana kufahamu, ikitokea ukaona kuwa uke wako unatoa harufu, kuuosha kwa maji mengi na sabuni nyingi mara nyingi, sio suluhisho bali unazidi kuleta matatizo zaidi kwa sababu unazidi kupunguza idadi ya bakteria wazuri, na kubadilisha hali ya utindikali wa uke na hivyo kukaribisha bakteria wabaya kwa wingi zaidi!!
-Na kitu cha mwisho ambacho ni muhimu zaidi, ni kwetu wanaume, unapoona mwenzi wako ana tatizo hili, usimseme vibaya au kumkaripia au kumtukana; Unatakiwa kutambua kuwa huo ni ugonjwa na umsaidie kuweza kuonana na wataalamu wa tiba kwa

Imechapishwa na jerry kwa 04:32 Hakuna maoni:
Tuma Hii kwa Barua pepeBlogu Hii!Chapisha kwenye XShiriki kwenye FacebookShiriki kwenye Pinterest
Lebo: burudani

Alhamisi, 12 Mei 2016

fahamu nchi zinazoongiza kwa ufisadi afrika

ImageWaziri mkuu wa Uingereza David Cameron alinaswa na kamera akiidunisha Nigeria kuwa mafisadi wakuu duniani

Baada ya waziri mkuu wa Uingereza David Cameron kunaswa na kamera akiidunisha Nigeria kuwa mafisadi wakuu kote duniani BBC imeamua kuangazia kwa umakini ikiwa matamshi hayo ni ya kweli.

Je Nigeria imeorodheshwa katika nafasi ipi katika orodha ya mataifa fisadi kwa mujibu wa shirikisho la kupambana dhidi ya ufisadi duniani Transparency International ?

ImageTanzania inaorodheshwa katika nafasi ya 117 duniani

Ni vigumu kuelezea kwa kina ama hata kupiga msasa ufisadi katika mataifa kwani kila mwanauchumi anaelezea ufisadi akitumia mizani tofauti na mwenziye.

Kwa sababu hiyo tutatumia orodha ya mwaka wa 2015 ya shirikisho la kupambana dhidi ya ufisadi, Transparency International, ili kukupa taswira ya mataifa ya kanda ya Afrika Mashariki na jinsi yanavyolinganishwa na mataifa mengine duniani katika mizani ya ubadhirifu na wizi wa mali ya uma.

Cha mno hata hivyo sharti tuweke bayana kuwa Nigeria sio taifa fisadi zaidi duniani.

ImageImageNigeria imeorodheshwa katika nafasi ya 136 Nigeria kati ya mataifa 167.

Nigeria imeorodheshwa katika nafasi ya 136 Nigeria kati ya mataifa 167.

Kenya kwa mfano inasemekana kuwa na ufisadi mkubwa hata kuishinda Nigeria.

ImageAPImageZimbabwe wanaorodheshwa katika nafasi ya 150 duniani kwa ufisadi.

Katika kanda ya Afrika Mashariki , mali ya umma inafujwa sana na viongozi wa serikali hali ambayo inaiweka mataifa ya kanda katika nafasi za mwisho mwisho kuashiria viwango vya juu vya ufisadi.

Kati ya mataifa kumi Fisadi zaidi duniani Somalia inaongoza ikifwatwa na Sudan ,Sudan Kusini, Eritrea, Burundi, DRC, Uganda, Kenya Tanzania Ethiopia na kisha Rwanda katika usanjari huo.

Somalia inaongoza kwa Ufisadi duniani katika nafasi ya 167.

Viwango vya ufisadi vinanasibishwa na Korea Kaskazini.

Nchi iliyojitenga kabisa na ufisadi kanda ya Afrika Mashariki na kati ni Rwanda.

ImageRwanda inaorodheshwa katika nafasi ya 44 duniani.

Taifa hilo linaloongozwa na rais Paul Kagame linaorodheshwa katika nafasi ya 44 duniani.

Je unakumbuka rais Robert Mugabe aliyewadunisha wakenya kwa kuwa wezi ?

Kulingana na orodha hii iliyotayarishwa na shirika la TI Zimbabwe wanaorodheshwa katika nafasi ya 150 duniani kwa ufisadi.

Wanagawana nafasi hiyo na Burundi.

Orodha ya mataifa 10 fisadi zaidi kanda ya Afrika Mashariki na Duniani.

1. 167 Somalia / Korea Kaskazini

2. 165 Sudan

3. 163 South Sudan/ Angola

4. 154 Eritrea/Yemen / Turkmenistan / Syria

5. 150 Burundi / Zimbabwe

6. 147 Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo / Chad / Myanmar /

7. 139 Kenya / Uganda

8. 117 Tanzania

9. 103 Ethiopia

10. 44 Rwanda

Imechapishwa na jerry kwa 00:16 Hakuna maoni:
Tuma Hii kwa Barua pepeBlogu Hii!Chapisha kwenye XShiriki kwenye FacebookShiriki kwenye Pinterest
Lebo: habari

Jumatano, 11 Mei 2016

msanii wa bongo movies afariki dunia

May 12 2016 ripoti zilianza kusambaa kwenye mitandao ya kijamii kwa baadhi ya mastaa wa filamu na Muziki nchini, kuhusiana nataarifa ya kufariki kwa mmoja kati ya wachekeshaji maarufu nchini Tanzania,  Mohammed Abdallah  (Kinyambe) kutoka kwenye maigizo ya Vituko Show.

Imechapishwa na jerry kwa 22:14 Hakuna maoni:
Tuma Hii kwa Barua pepeBlogu Hii!Chapisha kwenye XShiriki kwenye FacebookShiriki kwenye Pinterest
Lebo: celebrity

walimu walipwa kuku badala ya mshahara

ImageAFPImageWalimu walipwa kuku kama mshahara

Mji mmoja nchini Uzbekistan umekua ukiwapa waalimu wake kuku kama mshahara badala ya pesa. Mamlaka za mji wa Nukus katika jimbo linalojitawala la Karakalpakstan wamekua wakitia vifaranga wachanga kwa walimu kutokana na uhaba wa pesa nchini humo.

Kituo cha radio kinachofadhiliwa na Marekani{Radio Ozodlik} kimemnukuu mwalimu mmoja akilaani hatua hiyo kama aibu kubwa kwa mamlaka.

Mwalimu huyo aliyeghadhabishwa na hatua hiyo amesema hataki vifaranga kwa sababu anaweza kuwapata sokoni, lakini wanataka pesa zao.

Vifaranga wanaotolewa kama mshahara wana gharama ya dola mbili kila mmoja, ikiwa ni maradufu bei inayouzwa vifaranga sokoni.

Mamlaka za Uzbekistan hazikubalii uhuru wa vyombo vya habari na raia wa huko hutegemea vyombo vya habari vya kimataifa kutoa sauti yao, ila hawajitambulishi.

Uzbekistan imekumbwa na uhaba wa fedha kwa miaka sasa hali inayosababisha serikali kuchelewesha mishahara ya wafanyikazi na malipo ya uzeeni.

Mapema mwezi huu wafanyikazi wa serikali katika mji mkuu,Tashkent walilalamikia kwamba hawakuwa wamelipwa mshahara kwa miezi miwili kwa sababu benki hazikuwa na pesa.

Imechapishwa na jerry kwa 10:10 Hakuna maoni:
Tuma Hii kwa Barua pepeBlogu Hii!Chapisha kwenye XShiriki kwenye FacebookShiriki kwenye Pinterest
Lebo: habari

justin bieber sitapiga picha tena na mashabiki

ImageJustin Bieber asema hatopiga picha tena na mashabiki wake

Iwapo hujagundua basi ujue kwamba nyota wa muziki wa Pop Justin Bieber yuko katika ziara ya ulimwengu.

Kwa sasa yuko nchini Marekani ambapo alionekana amepumzika katika mbuga moja kabla ya tamasha yake mjini Boston.

ImageBieber alivyoandika katika mtandao wa instagram

Bieber ambaye alikuwa hana viatu aliwavutia mashabiki lakini akakataa kuzungumza nao hadi watakapoweka simu zao chini.

Haijulikani iwapo picha alizochukua na mashabiki wake katika lango la mbuga hiyo zilikuwa za mwisho,lakini baadaye jioni alichapisha katika mtandao wake wa Instagram kwamba hatapiga picha tena na mashabiki.

ImageHivi ndivyo mashabiki wake walivyomjibu

''Iwapo utakutana nami mahali ujue kwamba sitapiga picha tena'',aliandika.

Alielezea vile watu hawaezi hata kumsalimia ama kujua kwamba hata yeye ni binaadamu na hivyobasi kumfanya kujihisi kama mnyama na sasa anataka kuheshimiwa.

ImageTWITTERImageJustin Bieber aiwa nchini Marekani

Aliongezea: Najua kwamba watu hawatafurahia lakini hakuna mtu anayenidai picha.

Imechapishwa na jerry kwa 07:29 Hakuna maoni:
Tuma Hii kwa Barua pepeBlogu Hii!Chapisha kwenye XShiriki kwenye FacebookShiriki kwenye Pinterest
Lebo: celebrity

waziri mkuu atimuliwa bungeni

ImageGETTYImageWaziri mkuu wa New Zealand

Waziri Mkuu mpya wa New Zealand John Key ametupwa nje ya bunge na spika baada ya kukaidi kufuata kanuni za bunge.

Bunge hilo limekua na mjadala mkali kuhusu sakata ya akaunti za siri ambazo zinadaiwa kuwepo kisiwa cha Panama.

Spika wa Bunge David Carter ametetea hatua yake na kusema Waziri Mkuu alikaidi onyo la kutoheshimu kanuni za bunge, na hivyo hakua na kinga ila kumuadhibu, kama wabunge wengine.

Rekodi za bunge zimenakili kwamba Waziri Mkuu huyo aliwahi kutupwa nje ya bunge mara tatu wakati akiwa mbunge.

Hata hivyo si mara ya kwanza Waziri MKuu NewZealand anatupwa nje ya bunge.

Waziri Mkuu wa zamani Helen Clark alitupwa nje mwaka 2005 huku naye mtangulizi wake, David Lange akijipata pabaya miaka ya 1986 na 1987.

Imechapishwa na jerry kwa 07:22 Hakuna maoni:
Tuma Hii kwa Barua pepeBlogu Hii!Chapisha kwenye XShiriki kwenye FacebookShiriki kwenye Pinterest
Lebo: siasa

pengo la samatta laonekana tp mazembe

Mshambuliaji wa kimataifa Thomas Emmanuel Ulimwengu amesema kwamba kwa sasa pengo la Mtanzania mwenzake, Mbwana Ally Samatta linaonekana TP Mazembe.

Ulimwengu akiongea na Clouds FM alisema TP Mazembe kwa sasa inamkosa mshambuliaji mwepesi, mwenye uwezo wa kufunga kama Samatta.

Samatta ameondoka timu hiyo ya DRC Januari mwaka huu baada ya kushinda nayo taji la Ligi ya Mabingwa Afrika na kujiunga na KRC Genk ya Ubelgiji anakoendelea vizuri hivi sasa.

Tangu kuondoka kwa Samatta, Mazembe imeonekana kupoteza makali yake kiasi cha kuvuliwa mapema ubingwa wa Afrika.

Mazembe ilitolewa na Wydad Casablanca ya Morocco katika hatua ya 16 Bora ya Ligi ya Mabingwa na kuangukia kwenye kombe la Shirikisho.

Katika mechi iliyopita Mazembe ilipata ushindi mwembamba wa bao 1-0 katika mchezo wa kwanza wa mchujo kuwania kuingia hatua ya makundi ya Kombe la Shirikisho la Soka Afrika dhidi ya Stade Gabesien Uwanja wa Mazembe mjini Lubumbashi.

Ulimwengu aliyecheza kwa dakika 45 juzi kabla ya kutoka uwanjani akiwa anachechemea, alisema timu kwa sasa haina mtaalamu wa kufunga mabao kama alivyokuwa Samatta.

“Pengo la Samatta linaanza kuonekana sasa, pale mbele hakuna na anayeweza kufunga kama Samatta, tunapoteza nafasi nyingi sana, hilo ndilo tatizo,”amesema Ulimwengu.

Sasa Mazembe itakuwa na kazi ngumu katika mchezo wa marudiano wiki ijayo, ikitakiwa kwenda kuulinda ushindi huo mwembamba nchini Tunisia

Imechapishwa na jerry kwa 07:02 Hakuna maoni:
Tuma Hii kwa Barua pepeBlogu Hii!Chapisha kwenye XShiriki kwenye FacebookShiriki kwenye Pinterest
Lebo: michezo

chadema kuwasha moto nchi nzima

 

Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Vincent Mashinji Picha na Mtandao 

Kwa ufupi

Hiyo itakuwa mara ya kwanza kwa Chadema kufanya mikutano tangu baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 25, mwaka jana ambayo inalenga kukijenga na kuamsha ari ya wanachama tangu kilipokosa kura za kutosha kukiwezesha kushika dola.

Dar es Salaam. Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kinatarajia kuanza mikutano ya hadhara na ya ndani nchi nzima ili kujenga na kuinua uhai wake kuanzia Juni mwaka huu.

Hiyo itakuwa mara ya kwanza kwa Chadema kufanya mikutano tangu baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 25, mwaka jana ambayo inalenga kukijenga na kuamsha ari ya wanachama tangu kilipokosa kura za kutosha kukiwezesha kushika dola.

Miaka ya nyuma, Chadema ilipata umaarufu kupitia mikutano iliyopewa majina Operesheni Sangara na Vuguvugu la Mabadiliko (M4C).

Akizungumza na waandishi wetu juzi alipofanya ziara katika ofisi za gazeti hili zilizopo Tabata, Dar es Salaam, Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Vincent Mashinji alisema wapenzi wa chama hicho wakae mkao wa kusubiri mikutano iliyoandaliwa nchi nzima katika ngazi ya kanda.

“Kuanzia mwezi ujao tutaanza kuhakikisha watu hawasinzii. Kutakuwa na mikutano ambayo itakuwa inaratibiwa na kanda. Itategemea uzito wa ajenda ya hiyo kanda kisha watatujulisha sisi huku juu kama sekretarieti,” alisema Dk Mashinji.

“Kutakuwa na kazi nchi nzima, yale mambo ya kusema (Mwenyekiti wa Chadema Freeman) Mbowe yuko wapi leo hayatakuwepo tena. Kama ni Mtwara watakuwa huko na gesi yao, Bukoba watakuwa wanapambana na kahawa… nchi yote itakuwa kazini kwa sababu sisi tumegatua madaraka mikoani,” aliongeza.

Alipoulizwa watakuwa na ajenda gani baada ya ile ya ufisadi iliyowapa umaarufu kuporwa na Serikali ya Rais John Magufuli, Dk Mashindi alisema chama hakiendeshwi kwa ajenda za matukio, tu bali kwa itikadi na falsafa.

“Sidhani kama chama cha siasa kinaendeshwa kwa ajenda za matukio… Chama cha siasa kinaundwa na itikadi na falsafa. Hakipo kusubiri chama tawala kikosee ndipo kipate gia. Chama cha siasa kina kazi ya kueneza itikadi yake. Hapo ndipo mimi nataka kusimamia,” alisema.

Alipoulizwa kama atamudu kuvaa viatu alivyoviacha mtangulizi wake, Dk Willibrod Slaa, Dk Mashinji alijibu; “Viatu vya Dk Slaa, viko wapi nivipime? Wakati mwingine unamwangalia mtu anasema viatu vya Dk Slaa vikubwa, lakini mimi ndiye niliyekuwa injini yake. Najua unaweza kuwa injini ya mtu lakini ukipewa ile nafasi usiweze kufanya. Lakini ni kashfa gani aliyolipua Dk Slaa utakayouliza ambayo hatukuifanyia kazi?” alihoji.

Dk Mashinji alisema anaamini nafasi hiyo anaimudu. “Kwa asili binadamu huwa wanapenda kulinganisha watu. Dk Slaa alifanya mambo kwa wakati wake na mimi nitafanya kwa wakati wangu kuimarisha Chadema kuwa na uwezo kama taasisi,” alisema.

Akizungumzia hatua mbalimbali ambazo Chadema imepitia, Dk Mashinji alisema mikakati yao ni kukijenga chama kuanzia ngazi za chini na kutekeleza ahadi za wananchi katika majimbo, manispaa na halmashauri wanazoziongoza.

“Ukiangalia kama chama tunakwenda kwenye mabadiliko ya siasa na sasa tuko kwenye hatua muhimu sana. Tunaongoza halmashauri 24, hatuwezi kuendelea kuwa walalamikaji, bali watendaji,” alisema.

Alisema tangu walipokisajili chama hicho Januari 14, 1993 na kupewa hati ya usajili, kazi kubwa ilikuwa kujenga msingi. “Mwaka 1995 tuliweka wagombea wachache wa ubunge kwa sababu chama ndiyo kilikuwa kinakua. Tulipofika mwaka 2005 tukasema hapana. Lazima tukitangaze chama. Unapotangaza lazima pia ukiuze, tukamweka Mbowe. Akawa Mzee wa helikopta, akazunguka nchi nzima, ndiyo Chadema kikawa ndani ya watu,” alifafanua.

Alisema mwaka 2006, walianzisha programu ya Chadema ni Msingi iliyolenga kutoa elimu ya uraia. “Programu hiyo ilivuta watu wengi wakiwamo hata wa nje. Hapo ndiyo mlisikia ‘Chadema wanapewa hela na watu wa nje kutuoandoa madarakani’. Hapana, ilikuwa elimu ya uraia kabisa. Unawafundisha wananchi sheria za chama, Katiba inasemaje, huzungumzii chama hapo. Hiyo ni siku ya kwanza,” alisema.

Alisema siku ya pili walikuwa wakiitumia kuwafundisha Chadema ni nini, itikadi yao pamoja na mrengo wao.

“Sisi ni mrengo wa kati; kama unakuja na ubepari au ukomunisti hatujali. Falsafa yetu ni Nguvu ya Umma. Hata ukiangalia Katiba ndivyo inavyosema. Huwa tunasema tutawashtaki kwenye mahakama ya wananchi, kwa sababu ndiyo mahakama ya juu.”

Dk Mashinji alisema operesheni hii ya sasa itaendelea hadi mwaka 2019 wakati wa uchaguzi wa Serikali za Mitaa ili waweze kushinda na kujiandaa kwa Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2020.

“Tunapokwenda kwenye Uchaguzi wa Serikali za Mitaa, sera zitaonyesha kuwa hiki chama kimefikia hatua ya kushika dola,” alisema.

 

Imechapishwa na jerry kwa 05:12 Hakuna maoni:
Tuma Hii kwa Barua pepeBlogu Hii!Chapisha kwenye XShiriki kwenye FacebookShiriki kwenye Pinterest
Lebo: habari

sakata la sukari lachukua sura mpya

Dar es Salaam. Matumaini ya Watanzania kupata mgawo wa sukari yanazidi kufifia baada ya msako wa wafanyabiashara walioficha bidhaa hiyo kuchukua sura mpya kila uchwao.

Msako huo unaoendeshwa na maofisa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) kwa kushirikiana na polisi, ulianza baada ya Rais John Magufuli kutoa agizo hilo wiki iliyopita. Hata hivyo, licha ya kukamatwa sukari inayodaiwa kufichwa, imebainika kuwa baadhi ya waliohifadhi hawakuwa wameificha, bali walikuwa wanakamilisha taratibu za kodi na vibali.

Kutokana na hali hiyo, wafanyabiashara hao waliokuwa wanadaiwa kuficha zaidi ya tani 5,000, wamepewa ruksa ya kusambaza sukari hiyo na kuiuza kwa bei elekezi.

Miongoni hao ni Al-Neem Abdul Zacharia mwenye kampuni ya Al-Neem, ambaye kontena zake 70 zenye tani 1,840 za sukari zilidhaniwa kuwa zimefichwa bandarini.

Lakini jana, ilibainika kuwa taratibu za kutoa kontena hizo bandarini zilikuwa hazijakamilika.

Meneja wa kampuni hiyo, Zacharia Haroon alisema sukari hiyo ilinunuliwa Februari kutoka kwa kampuni ya Zenj General Traders na kibali kutoka Mamlaka ya Chakula na Dawa Tanzania (TFDA) kilipatikana juzi.

“Ilikuwa inasafirishwa Burundi lakini tukaomba tuinunue kwa sababu ya upungufu wa sukari hapa kwetu,” alisema.

Haroon ambaye ni baba wa mmiliki wa kampuni hiyo, alisema baada ya mwezi mmoja, kontena za sukari zilifika katika Bandari ya Dar es Salaam na taratibu za malipo ya kodi na kupewa kibali zilichukua muda mrefu ndiyo maana kontena hizo ziliendelea kubaki bandarini hadi walipopata kibali cha Serikali Mei 5 na cha TFDA juzi.

Alisema kwa sababu taratibu hizo zimekamilika sukari hiyo itaanza kusambazwa kwa wauzaji. “…Itauzwa kwa bei elekezi (Sh1,800),” alisema Haroon.

Maofisa wa Takukuru ambao wameagiza sukari hiyo isambazwe kwa wauzaji ndani ya saa 36, walisema kati ya kontena hizo, 30 zilikuwa katika Bandari ya Dar es Salaam na 40 katika bandari kavu ya Ubungo.

Kaimu Mkurugenzi wa Uchunguzi, Takukuru, Leonard Mtalai alisema walianza kufanyia uchunguzi taarifa za kuwapo kwa sukari hiyo baada ya chanzo chao kuwaeleza kuwa sukari hiyo ni mali ya Mbunge wa Mpendae Salim, Turky. Hata hivyo, Turky alisema hausiki na sukari hiyo.

Vilevile, sukari nyingine tani 4,900 iliyokuwa imekamatwa Mbagala imerejeshwa kwa mmiliki wake kwa ajili ya kuisambaza.

Mkurugenzi wa Huduma na Elimu ya Mlipakodi, Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Richard Kayombo alisema sukari hiyo imeachiwa kwa sababu mfanyabiashara huyo awali hakuwa amekamilisha baadhi ya taratibu, sasa zimekamilika.

Alisema kwa kipindi hicho, sukari ilikuwa kwenye maghala chini ya forodha.

“Amekamilisha taratibu za kodi, kibali cha Bodi ya Sukari na TFDA mwishoni mwa wiki,” alisema Kayombo na kuongeza kuwa baada ya kukamilisha taratibu hizo ametakiwa kuanza kusambaza sukari yake na kuuza kwa bei elekezi.

Serikali yaagiza tani 70,000

Serikali imeanza kupokea sukari kutoka nje, ikiwa ni sehemu ya tani 70,000 ilizoagiza ili kukabiliana na uhaba uliopo huku ikiwataka wasambazaji kuiuza kwa Sh1,800.

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ilisema jana kuwa tayari tani 11,957 zimeshawasili nchini na zitaanza kusambazwa leo kwenye mikoa yote.

Majaliwa ambaye aliondoka jana kwenda London, Uingereza kumwakilisha Rais Magufuli kwenye mkutano wa mapambano dhidi ya rushwa, alibainisha kuwa kutoka kwenye mzigo huo; tani 2,000 zitapelekwa mikoa ya Kaskazini, 3,000 Kanda ya Ziwa, 2,000 mikoa ya Kusini, tani 2,000 zitaelekezwa Nyanda za Juu Kusini. Mikoa ya Kanda ya Kati itapata tani 2, 000.

Alisema tani nyingine 24,000 zitawasili Ijumaa na kuanza kusambazwa kuanzia Jumatatu ijayo na mwishoni mwa mwezi huu au mwanzoni mwa Juni, Serikali itapokea tani nyingine 20,000.

Akamatwa na kilo 4,000

Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Dar es Salaam imekamata kilo 4,000 za sukari ilizosema zimefichwa katika eneo la Hananasif, Kinondoni mali ya Bushir Haroun.

Baada ya kukamatwa Haroun alisema: “Naona mmeniwahi, maana nilipanga leo kuitoa msaada katika kuelekea miezi ya Shaaban na mwezi Mtukufu wa Ramadhan.”

Imechapishwa na jerry kwa 05:07 Hakuna maoni:
Tuma Hii kwa Barua pepeBlogu Hii!Chapisha kwenye XShiriki kwenye FacebookShiriki kwenye Pinterest
Lebo: habari

mwanamke wa miaka 70, ajifungua mtoto

Baada ya miaka 46 ya ndoa, mwanamke mwenye miaka 70 amejifungua mtoto wa kwanza huko India.
.
Daljinder Kaur amejifungua mtoto wa kiume baada ya kupata matibabu ya IVF kwenye kliniki za uzazi huko India.

Kwenye picha akiwa na mume wake wa miaka 79, Kaur alisema yeye na mume wake walikuwa karibu kukata tamaa ya kupata mtoto kutokana na umri wao na kuona Kama Mungu amewalaani wasipate mtoto.

Alisema hatimae Mungu amejibu maombi yao na wamepata mtoto na sasa wanajiona wamekamilika.

Aliendelea kusema kuwa yeye na mume wake watamlea mtoto wao wenyewe kwasababu huyo mtoto amewapa nguvu mpya katika maisha. Pia anawasihii wote wenye changamoto za uzazi wamuombe Mungu bila kuchoka.... Aliongezea kusema....".....I can't wait to b a grandma!!

Imechapishwa na jerry kwa 04:45 Hakuna maoni:
Tuma Hii kwa Barua pepeBlogu Hii!Chapisha kwenye XShiriki kwenye FacebookShiriki kwenye Pinterest
Lebo: habari

magufuli yupo uganda

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli akiwasili katika Uwanja wa ndege wa Entebbe, nchini Uganda kwa ajili ya kuhudhuria sherehe za kuapishwa kwa Rais Yoweri Museveni, kesho.

Imechapishwa na jerry kwa 04:42 Hakuna maoni:
Tuma Hii kwa Barua pepeBlogu Hii!Chapisha kwenye XShiriki kwenye FacebookShiriki kwenye Pinterest
Lebo: habari

Jumanne, 10 Mei 2016

dangote kuwasaidia waathirika wa boko haram

ImageAFPImageDangote amewahi kutoa msaada awali kwa waathiriwa

Mtu tajiri zaidi Afrika Aliko Dangote ameahidi kutoa mamilioni ya pesa kusaidia waathiriwa wa mashambulio ya kundi la Boko Haram kaskazini mashariki mwa Nigeria.

Ameahidi kutoa $10m (£7m) kuwasaidia waathiriwa hao.

Mfanyabiashara huyo ametoa tangazo hilo baada ya kuzuru kambi za watu ambao wamelazimika kutoroka makwao kutokana na mashambulio ya kundi hilo la Kiislamu.

Bw Dangote awali alikuwa ametoa dola milioni sita kama msaada kwa watu hao.

ImagebImageDangote alitembelea kambi za wakimbizi

Miaka ya nyuma, wafanyabiashara wa Nigeria wametuhumiwa kwa kutotimiza ahadi wanazotoa za kutoa pesa za kuwasaidia waathiriwa.

Lakini afisa wa serikali nchini humo ameambia BBC kwamba, kwa mujibu wa ufahamu wake, Bw Dangote daima amekuwa akitimiza ahadi zake kwa waathiriwa.




Imechapishwa na jerry kwa 10:33 Hakuna maoni:
Tuma Hii kwa Barua pepeBlogu Hii!Chapisha kwenye XShiriki kwenye FacebookShiriki kwenye Pinterest
Lebo: habari

zungu achaguliwa kuwa mwenyekiti wa bunge


KUTOKA BUNGENI: Mbunge wa Jimbo la Ilala, Mussa Azzan Zungu amechaguliwa leo kuwa tena Mwenyekiti wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Akitoa neno la shukrani Zungu amesema nafasi hiyo sio rahisi lakini ataitumikia kwa uadilifu tena bila kupendelea upande wowote.

Imechapishwa na jerry kwa 10:27 Hakuna maoni:
Tuma Hii kwa Barua pepeBlogu Hii!Chapisha kwenye XShiriki kwenye FacebookShiriki kwenye Pinterest
Lebo: habari

serikali ya tenga 1trilioni kwa ajili ya wizara ya ulinzi

Mei 10 2016 Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa limewasilisha hotuba yake ya mapitio ya makadirio ya mapato na matumizi ya fedha kwa mwaka 2016/2017 ambayo imesomwa na Waziri wake Hussein Mwinyiambaye amesema…

>‘Wizara yangu inakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo kupatiwa kiwango pungufu cha fedha ikilinganishwa na mahitaji halisi ambayo ni makubwa’


‘Hali ya kutengewa bajeti ndogo na  fedha pungufu imekuwa ikiathiri utekelezaji wa mpango wa maendeleo ya Jeshi na pia kusababisha ulimbikizaji wa madeni hususani ya kimkataba ambayo tumeingia na makampuni mbalimbali kwa ajili ya kuliwezesha Jeshi kizana na kivifaa’

‘Mpango wa utekelezaji wa Wizara ya Ulinzi na Jeshi la kujenga Taifa wa mwaka 2016/2017 umekusudia kuimarisah utekelezaji kazi na ufanisi wa Jeshi kulingana na Dira na Dhima ya Wizara’

‘Ili Wizara ya Ulinzi na Jeshi la kujenga Taifa na Taasisi zake iweze kutekeleza majukumu yake ipasavyo katika mwaka 2016/2017 naliomba Bunge liidhinishe jumla ya shilingi 1,736,530,000.00 kwa ajili ya matumizi ya kawaida na matumizi mengine ‘

Imechapishwa na jerry kwa 09:40 Hakuna maoni:
Tuma Hii kwa Barua pepeBlogu Hii!Chapisha kwenye XShiriki kwenye FacebookShiriki kwenye Pinterest

uhaba wa sukari basi waziri mkuu

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amesema Serikali imeagiza Sukari kutoka nje ya nchi tani70,000 za sukari ambapo kati ya hizo, tani11,957 zimshawasili nchini na zitaanza kusambazwa kesho Mei 11, 2016.

Ametoa kauli hiyo leo mchana Mei 10, 2016wakati akizungumza na waandishi wa habari kwenye mkutano uliofanyika nyumbani kwake Oysterbay Dar es Salaam.

Akitoa ufafanuzi wa sukati ambayo imekwishawasili nchini Waziri Mkuu alisema tani 2000 zitapelekwa (Mikoa ya kaskazini), tani 3,000 (Mikoa ya kanda ya ziwa), tani 2,000 (Mikoa ya Kusini), tani 2,000 (Nyanda za Juu Kusini) na tani 2,000 (mikoa ya kanda ya kati).

‘Tani nyingine 24,000 za sukari zitawasili Ijumaa hii na hadi zitoke bandarini itakuwa kama Jumapili kwa hiyo zinaweza kusambazwa kuanzia Jumatatu.Tani nyingine 20,000 zitawasili baadaye, ama mwishoni mwa mwezi huu au mapema mwezi Juni’– Waziri Mkuu

Amesema anawataka watanzania wasihofu kuhusu uhaba wa sukari uliojitokeza hivi karibuni kwani umesababishwa na watu wachache ‘Mheshimiwa Rais ameagiza watu waliohodhi bidhaa hii wakamatwe na sukari isambazwa Lakini pia tunaagiza kwa muda mfupi kwasababu viwanda vyetu vinatarajia kuanza uzalishaji ifikapo Julai’- Waziri Mkuu

Waziri huyo amewataka wasambazaji wa sukari waziuze kwa wafanyabiashara wadogo ili wao wawauzie wananchi kwa bei elekezi ya Sh.1800, pia amewaagiza wakuu wa mikoa na wakuu wa wilaya kuhakikisha wanasimamia zoezi la ukaguzi ili kubaini zaidi wale waliohodhi bidhaa hiyo.

‘Serikali imetenga maeneo matatu yanayofaa kwa kilimo cha miwa huko Bagamoyo, Ngerengere na Kigoma huko wanaweza kulima na kujenga viwanda vya Sukari na uzalishaji ukawa unapanda mwaka kwa mwaka hadi utakapoweza kuimaliza hii gap iliyopo’- Waziri Mkuu

Imechapishwa na jerry kwa 09:36 Hakuna maoni:
Tuma Hii kwa Barua pepeBlogu Hii!Chapisha kwenye XShiriki kwenye FacebookShiriki kwenye Pinterest
Lebo: habari

kenya yakamata wanamgambo wa alshabab 36

ImagePSCU KenyaImageRais Uhuru Kenyatta wa Kenya

Vikosi vya usalama nchini Kenya vinasema kuwa vimewakamata washukiwa 36 wa kundi la wanamgambao wa al-Shabab tangu mwezi Septemba mwaka uliopita kulingana na gazeti la The Star nchini humo.

Washukiwa hao walikamatwa katika msitu wa Boni mashariki mwa raifa hilo.

Miezi tisa iliopita ,jeshi lilizindua operesheni Linda Boni kuwafurusha wanamgambo walioaminika kujificha katika msitu huo.

Kenya imekabiliwa na mashambulizi ya wapiganaji wa al-Shabab,ikiwemo shambulio mnamo mwezi Aprili 2015 katika chuo kikuu cha Garissa lililowauwa watu 148.

Imechapishwa na jerry kwa 07:57 Hakuna maoni:
Tuma Hii kwa Barua pepeBlogu Hii!Chapisha kwenye XShiriki kwenye FacebookShiriki kwenye Pinterest

nauli za kulipa daraja za kigamboni zipo hapa

Tayari Dar es salaam imeanza kufurahia urahisi wa kuvuka bahari kwa urahisi zaidi kwenye safari kati ya Kigamboni na Town Dar es salaam ambapo daraja lilivyozinduliwa tu tuliambiwa tutalipia ila hatukutajiwa bei, leo May 10 2016 ndio bei zimetajwa na unaweza kuzipata hapa chini.

Kaongea Injinia Joseph Nyamwuhanga kataja kila kitu >>> ‘Shughuli za kutoza fedha zitasimamiwa na shirika la NSSF na tumeweka tozo kwa watumiaji wa aina mbalimbali mfano Magari na Pikipiki na kila mmoja atalipa kulingana na aina ya chombo chake’

‘Kwa waendao kwa miguu wataendelea kupita bure mpaka Serikali itakapoweka utaratibu tofauti, wenye baiskeli tozo itakuwa shilingi 300/= ila kwa sasa watapita tu bure mpaka tutakapowatangazia siku ya kuanza kulipa, kwa wenye pikipiki watalipa shilingi 600/=, Baiskeli za miguu mitatu (Guta) watalipa shilingi 1500/=’  

‘Mikokoteni watalipa shilingi 1500/=, Pikipikiza Miguu mitatu ambazo ni Bajaji watalipa Tsh. 1500/=, Gari ndogo (Saloon Cars) watalipa kwa shilingi 1500/= Magari aina ya Pick-Upyasiyozidi tani mbili yatalipa shilingi 2000/=, (Minibuses) mabasi madogo yanayobeba abiria wasiozidi 15 yatalipa shilingi 3000/=,Mabasi yanayobeba abiria kati ya 15 -29 yatalipia Tsh. 5000/=, Tractor ni Tsh. 7000/= 

‘Tractor yenye trailer lake hao watalipa shilingi 10,000/=, Magari yenye uzito wa tani 2 mpaka 7 watalipia 7000/=, magari yenye uzito wa tani 7 mpaka 15 watalipia 10,000/=, magari yenye uzito wa tani 15 mpaka 20 watalipia 15,000/=, magari yenye tani  20 mpaka 30 watalipia shilingi 20,000/=, Semi  Trailer kama magari yanayobeba mafuta  yatalipia 30,000/=, Truck Trailer watalipia shilingi 30,000/=,

Imechapishwa na jerry kwa 07:52 Hakuna maoni:
Tuma Hii kwa Barua pepeBlogu Hii!Chapisha kwenye XShiriki kwenye FacebookShiriki kwenye Pinterest
Lebo: habari

ajifungua mapacha watano

ImageWatoto Keith, Ali, Penelope, Tiffany na BeatrixMama mmoja raia wa Australia ametoa picha za mapacha watano aliowazaa mwezi Januari.

Kim Tucci wa miaka 26 alichukua dadika mbili tu kujifungua wanawe hao, wasichana wanne na mvulana mmoja.

Wote walitungwa kawaida, hakutumia matibabu yeyote ya uzazi.

ImageFamilia inasema watoto huvishwa vibinda 350 kwa wiki

Madaktari 50 walimsaidia mama huyo kujifungua kwa njiya ya upasuaji, na wanawe wote wako shwari.Wanasayansi wanasema ni mama mmoja kati ya milioni 55 ana nafasi ya kuzaa mapacha watano.

Bi Tucci alipata umaarufu sana wakati alipoweka taarifa za mimba yake katika ukurasa wake wa Facebook.Kampuni ya kunasa picha ya Erin Elizabeth imesaidia sana kunadi safari ya Bi Tucci wakati wa uja uzito wake.

ImageKim Tucci akiwa mja mzito na pacha wake

Mama huyo ameelezea changamoto alizokumbana nazo akisema kwa wakati mmoja alihisi kama anapoteza maisha.Ameongeza madaktari walimshauri kuwaokoa watoto wawili na kumtaka kuwatoa wengine kutokana na sababu za kiafya.

Hata hivyo aliamua kubeba mimba yake hadi mwisho.

Bi Tucci na mumewe bwana Vaughn wana watoto watatu mvulana na wasichana wawili.Wameanza kuchangisha pesa ili kununua gari kubwa ambalo litaweza kukimu familia hiyo kubwa.

Imechapishwa na jerry kwa 05:42 Hakuna maoni:
Tuma Hii kwa Barua pepeBlogu Hii!Chapisha kwenye XShiriki kwenye FacebookShiriki kwenye Pinterest
Lebo: UDAKU

amir khan sitapigana na kell brook

Amir Khan: Sitapigana na Kell Brook

ImageAFPImageAmir Khan

Bondia Amir Khan amesema hakuna uwezekano wowote wa yeye kuchuana na mpinzani wake mkuu Kell Brook, licha ya kushindwa vibaya na Saul Canelo Alvarez.

Kulikuwa na matumaini makubwa kuwa kufuatia uamuzi wake wa kujiunga katika uzani wa Kati au Middleweight, pigano kati yake na bingwa wa shirisho la kimataifa la dondi IBF, Kell Brook, lingeandaliwa.

Lakini Khan amesema Brook sio bondia mwenye tajiriba na kwa sasa hawezi kushiriki pigano lolote dhidi yake.

Amesema anamheshimu bondia huyo, kwa sababu ni bingwa wa dunia lakini tofauti zao haziwezi kumruhusu kukubali pigano lolote naye.

'' Ningependa kupambana na mabondia mashuhuri duniani, ili kuwa na rekodi nzuri na kwa sasa nimesalia na mapigano machache tu'' Alisema Khan.

ImageBondia Kell Brook

Khan anayetoka eneo la Bolton na Brook kutoka Sheffield wamekuwa wakitaniana kwa muda na wakati Brook aliposhinda taji la dunia pigano dhidi yao likionekana kukaribia.

Lakini baada ya kutokuwa na taji lolote la dunia, na kupoteza kwa mara ya nne tangu mwaka wa 2012, Khan anasema Brook sio bondia wa kiwango chake.

Khan mwenye umri wa miaka 29, huenda sasa anapimana nguvu na Mmarekani Danny Garcia, bingwa wa shirikisho la WBC, ambaye alimshinda kwa njia ya knockout miaka minne iliyopita.

Imechapishwa na jerry kwa 04:46 Hakuna maoni:
Tuma Hii kwa Barua pepeBlogu Hii!Chapisha kwenye XShiriki kwenye FacebookShiriki kwenye Pinterest

mabasi ya mwendo kasi yaanza

ImageMabasi ya mwendo wa kasi TZ

Huduma ya mabasi ya uchukuzi yanayoenda kwa kasi BRT nchini Tanzania imeanza rasmi siku ya jumanne katika jiji la kibiashara la Dar es Salaam.

Abiria watalipa shilingi 400 na 800 huku wanafunzi wakilipa 200 kulingana na mamlaka ya uchukuzi wa barabarani na majini SUMATRA.

ImageKituo cha mabasi ya mwendo wa kasi Tanzania

Mkurugenzi mkuu anayesimamia mamlaka hiyo bw Giliard Ngewe amewaambia maripota mjini humo kwamba nauli zitakuwa shilingi 400 kwa uchukuzi wa barabara ndogo,650 kwa barabara kuu na shilingi 800 kwa uchukuzi wa barabara kuu na ndogo huku wanafunzi wakilipa shilingi 200 kwa kila safari.

ImageAbiria wakiwa wamepanda basi la BRT

ASiku ya Jummanne na Jumatano mabasi hayo yatahudumu kati ya saa kumi na moja alfajiri na saa sita mchana.

ImageKituo cha mabasi ya BRT Tanzania

Tunawaonya wanaoendesha pikipiki na madereva wa magari mengine kutotumia barabara za mradi wa BRT,alisema akiongezea kwamba bado wanazungumza na washikadau kutafuta njia nzuri ya kupanga barabara zitakazotumiwa na BRT na mabasi mengine ya abiria.

Kulingana na yeye,mfumo huo wa BRT hauyaruhusu mabasi mengine kutoa huduma pamoja na mabasi ya BRT kwa hivyo abiria walioko katika barabara za BRT hawataruhusiwa kutumia mabasi mengine.

Imechapishwa na jerry kwa 04:40 Hakuna maoni:
Tuma Hii kwa Barua pepeBlogu Hii!Chapisha kwenye XShiriki kwenye FacebookShiriki kwenye Pinterest
Lebo: habari

Lipumba uhaba wa sukari umesababishwa na magufuli

Akihojiwa na Mtangazaji Yvonne Kamuntu kwenye Azam News, Mchumi mbobezi hapa nchini Prof. Ibrahim Haruna Lipumba amesema uhaba wa sukari uliopo kwa sasa nchini umesababishwa na Rais John Magufuli mwenyewe kwa kuzuia sukari ya nje kutoingizwa Nchini, ilhali viwanda vyetu havikidhi idadi inayohitajika katika uzalishaji wake.

Pia Prof. Lipumba amesema hakuna sheria inayoruhusu Serikali au Bodi ya Sukari kupanga bei ya sukari nchini hivyo ametaka siasa kuacha kutumika katika mambo serious na wafanyabiasahara wasitishwe.

Imechapishwa na jerry kwa 04:21 Hakuna maoni:
Tuma Hii kwa Barua pepeBlogu Hii!Chapisha kwenye XShiriki kwenye FacebookShiriki kwenye Pinterest
Lebo: habari

mkuu wa wilaya ya kinondoni afanya tena safari y kushtukiza

May 10 2016 Mkuu wa wilaya ya kinondoni, Ally Hapi amefanya ziara ya kushtukiza asubuhi na mapema majira ya saa kumi na mbili  katika hospitali ya Sinza Palestina na kujionea changamoto zinazoikabili Hospitali hiyo.

Baadhi ya changamoto ambazo amezikuta Hospitalini hapo ni pamoja na wagonjwa kukosa neti kwenye vitanda, upungufu wa dawa na kukosekana kwa jenereta lenye nguvu la kuendeshea vifaa vinavyotumia umeme mwingi hivyo kushindwa kutoa huduma pindi umeme unapokatika.

Mkuu huyo wa wilaya anatarajia kukaa na uongozi wa Hospitali zote za serikali zilipo wilaya ya kinondoni kuona namna ya kutatua changamoto zinazowakabili.

.

Jenereta ambalo huwa linatumika pindi umeme unapokatika lakini halina nguvu ya kuendeshea vifaa vinavyotumia umeme mwingi hivyo kushindwa kutoa huduma.

Umeme wa Nishati ya jua ambao pia hauna nguvu ya kuendeshea vifaa vinavyotumia umeme mwingi hivyo kushindwa kutoa huduma pindi umeme unapokatika

.

.

.

.

.

.

.

.

.

Imechapishwa na jerry kwa 04:10 Hakuna maoni:
Tuma Hii kwa Barua pepeBlogu Hii!Chapisha kwenye XShiriki kwenye FacebookShiriki kwenye Pinterest
Lebo: habari

polisi waandamana kisa beyonce

ImageGettyImageBeyonce Knowles

Kundi moja la maafisa wa polisi limefanya maandamano karibu na tamasha lililofanyika katika mji wa nyumbani wa nyota wa muziki Beyonce huko Houston.

Wanachama wa muungano wa polisi na Sherrif walisimama mbali na uwanja wa soka na kuelekeza mwangaza wa bluu katika ukumbi wa tamasha hilo.

Walikuwa wanapinga kanda ya video ya Beyonce ambayo wanasema inawaponza polisi.

ImageReutersImageMaafisa wa polisi wa Marekani

Mwanamuziki huyo tayari amesema kwamba hawakosoi polisi katika wimbo huo na kusema kuwa maafisa wa polisi wanaodhani aliwaponza wanakosea.

Mwanachama mmoja wa polisi amekiambia chombo cha habari KHOU11 kwamba hawakufurahia baada ya Beyonce kutumia picha za gari moja la polisi mjini New Orleans iliokuwa ikizama katikamafuriko.

''Tunaamini kwamba baadhi ya mambo yake ni kinyume na maafisa wa polisi'',alisema.

ImageBeyonce_black_Panther

Mnamo mwezi Aprili,Beyonce aliambia jarida la Elle kwamba anaheshimu polisi lakini hapendi unyanyasaji.

''Mtu yoyote anyedhani kwamba siwapendi polisi anakosa kwa sababu'', alisema.

''Ninawapenda na kuwaheshimu sana polisi pamoja na familia za maafisa hao ambao hujitolea ili kuhakikisha tuko salama''.

Imechapishwa na jerry kwa 03:44 Hakuna maoni:
Tuma Hii kwa Barua pepeBlogu Hii!Chapisha kwenye XShiriki kwenye FacebookShiriki kwenye Pinterest
Lebo: celebrity
Machapisho Mapya Machapisho ya Zamani Nyumbani
Jisajili kwenye: Maoni (Atom)

Ads Inside Post

statistics

Subscribe

Formulir Kontak

Jina

Barua pepe *

Ujumbe *

Kunihusu

jerry
Tazama wasifu wangu kamili

Kumbukumbu la Blogu

  • ►  2017 (126)
    • ►  Machi (114)
    • ►  Februari (9)
    • ►  Januari (3)
  • ▼  2016 (93)
    • ▼  Desemba (2)
      • ifahamu kensa
      • uke kutka harufu mbaya
    • ►  Mei (91)
      • fahamu nchi zinazoongiza kwa ufisadi afrika
      • msanii wa bongo movies afariki dunia
      • walimu walipwa kuku badala ya mshahara
      • justin bieber sitapiga picha tena na mashabiki
      • waziri mkuu atimuliwa bungeni
      • pengo la samatta laonekana tp mazembe
      • chadema kuwasha moto nchi nzima
      • sakata la sukari lachukua sura mpya
      • mwanamke wa miaka 70, ajifungua mtoto
      • magufuli yupo uganda
      • dangote kuwasaidia waathirika wa boko haram
      • zungu achaguliwa kuwa mwenyekiti wa bunge
      • serikali ya tenga 1trilioni kwa ajili ya wizara ya...
      • uhaba wa sukari basi waziri mkuu
      • kenya yakamata wanamgambo wa alshabab 36
      • nauli za kulipa daraja za kigamboni zipo hapa
      • ajifungua mapacha watano
      • amir khan sitapigana na kell brook
      • mabasi ya mwendo kasi yaanza
      • Lipumba uhaba wa sukari umesababishwa na magufuli
      • mkuu wa wilaya ya kinondoni afanya tena safari y k...
      • polisi waandamana kisa beyonce

Popular

  • Historia ya Sarafu Yetu Tanzania
    Nimesikia kuwa hivi karibuni, nchi zote za Afrika ya Mashariki zitatumia sarafu moja. Nimekuwa natafiti pole pole kutafuta picha za pesa tul...
  • PICHA 12 ZA UTUPU ZA WASANII NA WAIGIZAJI WA BONGO
    HUYU NI ARVIL HUYU NI ARVIL 2 MLIMBWENDE MWINGINE NI HUYU HAPA ANITWA JACK PATRICK   NAE PICHA ZAKE ZILI MAKE ...
  • Kushamiri kwa makundi ya biashara za ngono kupitia mitandaoni, serikali iko wapi
    Leo kuna jambo napenda tulijadili kama jamii kupitia hapa kwenye jukwaa letu lenye hadhi kitaifa na kimataifa. Niende kwenye mada, nimekua m...
  • nauli za kulipa daraja za kigamboni zipo hapa
    Tayari Dar es salaam imeanza kufurahia urahisi wa kuvuka bahari kwa urahisi zaidi kwenye safari kati ya Kigamboni na Town Dar es salaam am...
  • nafasi za kazi
    Job Opportunity- Financial Controller, Application Deadline: 14 May 2016 VACANCY Our Client; is a private liability Pan- African Company...
  • Mafuta ya Habbat Soda ni Dawa kwa Kila Ugonjwa Isipokuwa Kifo..!!!
    Inapotokea wafalme wa Misri, Malkia wa Ulaya, Mitume na wanasayansi wa kisasa wanakuja na kukubaliana katika jambo moja, ni mhim...
  • SMS ZA MAPENZI KWA MPENDAE
    Ni kitu muhimu sana katika maisha ya uhusiano kwani zinatia chachu na kumfanya mwenza wako ajihisi ni wa pekee katika kichwa chako,kwamba ...
  • InstagramNEWS: Ni staa gani wa bongo kafuta picha zote Instagram? kisa?
    Asteria ni mtangazaji mpya wa AyoTV , kazi yake nyingine ni kukusogezea habari kubwa...
  • fursa kwa wale wanaopenda kwenda ulaya
    Utafutaji wa Watanzania kwenda ulaya au nje ya nchi kutafuta maisha umekua kwa kasi sana hivi sasa. Thread nyingi sasa hapa JF zina watu...
  • Chadema yaweka ulinzi mkali nyumba ya mama Wema......Ni Baada ya Nyumba Hiyo Kupigwa Mawe Usiku
    Nyumba ya mama Wema Sepetu, Mariam Sepetu, iliyopo Sinza Mori jijini Dar es salaam usiku wa kuamkia jana imepigwa mawe juu ya bati k...

Label

  • BREAKING news
  • burudani
  • celebrity
  • habari
  • michezo
  • mitandao ya kijamii
  • siasa
  • UDAKU
  • video
  • zote

Comment

Recent

Mandhari ya Rahisi. Inaendeshwa na Blogger.